Connect with us

News

Mwandishi wa Vitabu vya Tamthilia Ngugi wa Thiong’o amefariki

Published

on

Mwandishi nguli wa vitabu vya tamthilia Ngugi wa Thiong’o ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 87.

Familia imethibitisha kifo chake kilichotokea siku ya Jumatano Mei 28, 2025 nchini Marekani.

Ngũgĩ wa Thiong’o ni mmoja wa waandishi mashuhuri na wenye ushawishi mkubwa kutoka Afrika, hasa nchini Kenya. Anafahamika sana kwa maandishi yake ya kifasihi, hasa Riwaya, Tamthilia, Insha na tafakari kuhusu Lugha, Siasa, Utamaduni na Ukoloni.

James Ngugi wa Thiong’o, baadaye alijulikana kama Ngũgĩ wa Thiong’o baada ya kuacha jina la Kikristo.

Alizaliwa  tarehe 5 Januari 1938 katika kijiji cha Kamĩrĩthũ, eneo la Limuru katika kaunti ya Kiambu.

Ngugi alisoma katika shule ya upili ya Alliance High School – mojawapo ya shule za kitaifa nchini Kenya, kisha akaelekea katika chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda na kuhitimu mwaka 1963 na akajiunga na chuo kikuu cha Leeds nchini Uingereza ambako aliendelea na masomo yake ya fasihi.

Ngũgĩ alianza kuandika vitabu katika lugha ya Kiingereza lakini baadaye aliacha kutumia Kiingereza katika kazi zake za fasihi na kuanza kuandika kwa lugha za Kikuyu na Kiswahili, kama njia ya kuendeleza utamaduni na lugha za Kiafrika.

Baadhi ya vitabu vyake maarufu ni pamoja na Weep Not, Child (1964) – riwaya ya kwanza ya Mwafrika kuchapishwa kwa Kiingereza.
Vingine ni pamoja na The River Between (1965), A Grain of Wheat (1967), Petals of Blood (1977), Devil on the Cross (Caitaani Mutharaba-ini, 1980) – aliandika akiwa gerezani, kwenye karatasi za chooni na Matigari (1986) – kitabu hiki kilipigwa marufuku Kenya kwa sababu ya ujumbe wake wa mapinduzi.

Baada ya vitisho vya kisiasa na kushambuliwa nchini Kenya, Ngũgĩ alihamia Uingereza, kisha Marekani, ambako ameendelea kufundisha katika vyuo vikuu mbalimbali hadi kifo chake.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mwanaharakati Mwabili Mwagodi apatikana

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Mwabili Mwagodi ambaye alidaiwa kutekwa nyara akiwa nchini Tanzania sasa amepatikana.

Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za kibinamu nchini la VOCAL Africa Hussein Khalid, alisema Mwabili alipatikana katika msitu wa Kinondo eneo bunge la Msambweni kaunti ya Kwale mwendo wa saa tisa usiku akitembea kuelekea Diani.

Khalid alisema Mwabili, anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya mjini Mombasa kisha baadaye atasafirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi kuungana na familia yake.

“Tunashukuru Mwabili amepatikana akiwa hai japo amedhohofika na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya na kisha atarudi Nairobi kukutana na familia yake lakini tunaiambia serikali ya Kenya na Tanzania ni lazima wahusika kukomesha tabia hii ya kuwateka watu nyara kuna sheria kama mtu amekosea apelekwe Mahakamani”, alisema Khalid.

Hata hivyo Wanaharakati hao wa kutetea haki za kibinadamu waliishtumu serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuwanyanyasa wanaharakati wa kijamii wa taifa la Tanzania na wale wanaoingia Tanzania kutoka mataifa mengine ili kuendeleza hamasa za haki za kijamii.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Herman yahairishwa

Published

on

By

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara ambaye ni raia wa Uholanzi, Rowenhorst Herman na mlinzi wake Evans Bokoro imeahirishwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu kufuatia Mahakama kuingia kwenye mapumziko rasmi ya majaji.

Mke wa Marehemu, Riziki Cherono pamoja na mshukiwa mwenza Timothy Omondi wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga na kutekeleza mauaji hayo yaliyotokea Juni 4 mwaka 2021 katika eneo la Shanzu kaunti ya Mombasa.

Katika kikao cha awali cha Mahakama, Afisa wa Polisi Koplo Richard Cheruiyot alieleza mbele ya Jaji Wendy Micheni kwamba Cherono alijaribu kuonekana kama mwathirika kwa madai ya kutekwa nyara na majambazi waliodaiwa kuvamia nyumba yao.

Afisa huyo alieleza kwamba walimkuta Cherono akiwa amefungwa kwenye usukani wa gari lake, huku akidai kwamba alivamiwa na kulazimishwa kuondoka nyumbani kwao akiwa chini ya tishio la bunduki.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa ulibaini kwamba Marehemu Herman alipatikana amefariki nyumbani kwake akiwa amefungwa mikono na miguu huku mlinzi wao, Evans Bokoro, alikutwa akiwa hai kwa taabu karibu na bwawa la kuogelea lakini baadaye alifariki akipelekwa hospitalini.

Mashahidi wa upande wa mashtaka pamoja na polisi, wanaamini kwamba Cherono ndiye mshukiwa mkuu wakidai kwamba alipanga na kufanikisha mauaji hayo kwa kushirikiana na watu wengine, wakiwemo waliotajwa kuwa sehemu ya genge lililovamia nyumba hiyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending