Connect with us

News

Mwanamume auwawa na Ndovu -Kavunzoni Ganze

Published

on

Maafisa wa usalama kwa ushirikiano na wale Shirika la huduma kwa wanyamapori nchini KWS, wamewatahadhari wananchi kuwa waangalifu dhidi ya Wanyamapori hasa Ndovu katika eneo la Ganze.

Hii ni baada ya Mwanaume mmoja kuuwawa na Ndoa, mchana wa Alhamis Agosti 14, 2025 katika maeneo ya Kavunzoni wadi ya Bamba eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.

Kulingana na taarifa ya Polisi jamaa huyo aliyefahamika kwa jina la Stephen Rimba Gonja, anadaiwa kuwa mwalimu mstaafu wa shule ya msingi ya Kavunzoni alivamiwa na Ndovu akiwa shambani kwake na kutungwa pembe hadi akafariki.

Pembe ya Ndovu iliyovunjaka baada ya Ndovu kumuua mwanamume mmoja

Tayari maafisa wa KWS wameanzisha doria katika maeneo hayo kuhakikisha Ndovu wote walitangana na binadamu wanarudishwa mbugani.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending