Business
Muungano wa Tuktuk Kwale wapendekeza kutengewa sehemu maalum ya maegesho

Muungano wa waendeshaji wa tuktuk katika kaunti ya Kwale umetaka serikali ya kaunti hiyo kuwatengea sehemu maalum ya kudumu ya maegesho.
Madereva hao walisema kuwa sekta hiyo imekuwa ikichangia pakubwa kwa ukuaji wa uchumi wa kaunti hiyo na kuchangia kiasi kikubwa cha ushuru unaokusanywa na serikali.
Walisisitiza kuwa tuktuk zimekua zikisaidia kusafirisha watalii kufika maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii na iwapo wataimarishiwa mazingira ya kazi kutachangia kuimarisha sekta ya utalii pamoja na kuinua maisha ya vijana wengi wanaotegemea kazi hiyo kujikimu kimaisha.
Muungano huo pia ulisema ikiwa hayo yatatiliwa maanani huenda sekta hiyo ya uchukuzi ikaimarika kimapato kwa asilimia pamoja na uchumi wa kaunti hiyo
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Business
KPA kushirikiana na kaunti ya Siaya kibiashara

Halmashauri ya bandari Kenya (KPA) pamoja na serikali ya kaunti ya Siaya zimeahidi kushirikiana kwa karibu kuimarisha miundomsingi ya usafiri na biashara katika ukanda wa Ziwa Victoria.
Katika kikao cha viongozi wa pande zote mbili kilichofanyika jijini Mombasa, viongozi hao walijadili miradi ya miundomsingi ya baharini inayolenga kufungua fursa mpya za uwekezaji na mageuzi ya kiuchumi kwa wakazi wa maeneo ya Ziwa Victoria.
Mkurugenzi mkuu wa KPA nahodha William Ruto alithibitisha kuwa usanifu wa kivuko cha Usenge utakamilika ndani ya wiki mbili, huku ikiahidi kushirikiana na Kenya Shipyards Limited kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa wakati.
Aidha, Ruto alieeleza utayari wa mamlaka hiyo kushirikiana na serikali ya kaunti ya Siaya kuhakikisha miradi hiyo inaendana na vipaumbele vya eneo hilo.
Ruto aliongeza kuwa miradi hiyo inalenga kuchochea uwekezaji, kuongeza nafasi za ajira na kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika ukanda wa ziwa.
Kwa upande wake, gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo alieleza kuridhishwa na ushirikiano huo, akimpongeza nahodha Ruto kwa uongozi wake wa vitendo akisema kuwa miradi hiyo inaleta matumaini mapya kwa wakazi wa Siaya na ukanda mzima wa Ziwa Victoria.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Business
Wadau wa sekta ya uvuvi walalamikia unyakuzi wa ardhi

Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uchumi wa bahari na masuala ya ubaharia imewataka wawekezaji wote waliovamia ardhi zilizotengewa
Kauli hii ilijiri baada ya wavuvi na wasimamizi wa fuo za bahari kuelekeza lalama zao kwa kamati hiyo wakidai kuhangaishwa kila mara na baadhi ya mabwenyenye wanaodaiwa kushirikiana na baadhi ya maafisa wa serikali.
Walidai kwamba unyakuzi huo umekuwa donda sugu na uliadhiri pakubwa shughuli za uvuvi huku wakiitaka serikali ya kitaifa kuingilia kati na kuhakikisha ardhi hizo zinarudhishwa mikononi mwa jamii za wavuvi haraka iwezekanavyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo na ambaye pia ni mbunge wa Marakwet Mashariki David Kangogo Bowen alisema ujenzi wa kibinafsi katika maeneo ya mita 60 kutoka ukingo wa bahari ni ukiukaji wa sheria kwani maeneo hayo yametengwa mahususi kwa matumizi ya wavuvi.
“Wale wamejenga mita 60 kando ya bahari waondolewa ndio hawa wavuvi wapewe nafasi ya kufanya biashara yao vizuri na pia wapate sehemu ya kuegeza maboti yao”. … alisisitiza David Bowen.
Kauli yake iliungwa mkono na mbunge wa Matunga Kassim Sawa Tandaza aliyesema agizo hilo ni sharti litekelezwa mara moja na yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Taarifa ya Elizabeth Mwende