Connect with us

National News

Muturi Atemwa Katika Baraza la Mawaziri

Published

on

Rais William Ruto amefanya mabadiliko kadhaa katika baraza lake la mawaziri na kuwateua watu wengine kushikilia nyadhfa hizo huku aliyekuwa Waziri wa utumishi wa umma nchini Justin Muturi akitemwa nje.

Katika chapisho rasmi la gazeti la serikali ambalo limetiwa saini na mkuu wa utumishi wa umma nchini Felix Koskei, Rais Ruto kwa kuzingatia kipengele cha 152 ibara ya 2 ya katiba, amemteua Hanna Wendot Cheptumo kushikilia Wizara ya Jinsia, utamaduni na turathi.

Mwengine ni Mbunge wa Mbeere Geoffrey Kiringa Ruku ambaye ameteuliwa kushikilia Wizara ya utumishi wa umma nchini, Wizara ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Justin Muturi ambaye ametemwa nje ya baraza la mawaziri.

Kiongozi wa taifa, ametumia mamlaka yake ya kikatiba kwa kuzingatia kipengele cha 152 ibara ya 5{a}, na kufanya uhamisho wa mawaziri kutoka Wizara moja hadi nyingine ambapo Waziri wa mazigira na misitu nchini Adan Duale amehamishiwa Wizara ya Afya nchini huku Deborah Barasa ambaye alikuwa akishinikilia Wizara hiyo akihamishiwa Wizara ya Mazingira na misitu.

Uteuzi huo mpya wa mawaziri pamoja na uhamisho, umejiri siku moja tu baada ya Rais Ruto kufanya kikao na viongozi kutoka mlima Kenya pamoja na viongozi wengine kutoka maeneo ya Magharibi mwa Kenya sawa na kikao tofauti na Viongozi wa kidini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending