Connect with us

International News

Musevani ateuliwa kuwania urais Uganda mwaka 2026

Published

on

Chama tawala nchini Uganda, cha National Resistance Movement (NRM), kimemteua Rais Yoweri Museveni kuwa mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2026.

Akizungumza baada ya uteuzi huo uliofanyika katika makao makuu ya Tume ya uchaguzi ya chama cha NRM mjini Kampala, Rais Museveni alisema atazingatia zaidi masuala ya kuinua uchumi wa jamii na maendeleo.

Museveni alisema iwapo atachaguliwa tena kuliongoza taifa hilo basi atahakikisha Uganda inaendelea kushuhudia maendeleo licha ya kutawala taifa hilo kwa zaidi ya miaka 40 tangu mwaka wa 1986.

Japo taifa la Uganda limekuwa likiandaa chaguzi za kidemokrasia, Rais Museveni alishtumiwa kwa kukandamiza upinzani na kuendeleza utawala wa kidikteta.

Museveni na mkewe Janet wakiwasili katika makao makuu ya NRM

Akiwa uingozini, Rais Museveni alishinikiza kufanyika kwa mabadiliko Katiba ya nchi hiyo, kwanza mnamo mwaka wa 2005 kuondoa umri unaoruhusu mtu kuwania kiti cha urais nchini humo na kisha mnamo mwaka wa 2017, katiba hiyo ikafanyiwa marekebisho kufutiliwa mbali vipindi vya kiutawala.

Kufuatia hatua hiyo, sasa Museveni ana nafasi nzuri ya kuwania tena kiti cha Urais mwaka ujao wa 2026 wakati w auchaguzi mkuu nchini humo.

Upinzani ulishtumu vikali hatua hiyo ukisema ni ukiukaji wa Katiba huku Mpinzani mkuu nchini humo Kizza Besigye yuko korokoroni akikabiliwa na shtaka la uhaini ingawa hali yake ya afya inatajwa kuendelea kudhofika.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Matumaini ya kusitisha vita Gaza yaanza

Published

on

By

Licha ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kwamba mpango wa usitishaji mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa Gaza unakaribia, kundi la Hamas limeeleza kwamba bado mazungumzo yanaendelea.

Katika kile kinachoonekana kama jibu la kwanza la Hamas tangu Rais Trump kutangaza kupatikana kwa mwafaka huo, kundi hilo lilisema kwamba bado linaendelea kuyatafakari mapendekezo mapya yaliyomo kwenye mpango huo.

“Tunalichukulia suala hili kwa uangalifu mkubwa. Tunafanya majadiliano ya kitaifa kuyatathmini mapendekezo ya ndugu zetu wapatanishi”, lilisema kundi hilo kupitia Kiongozi wao.

Mnamo siku ya Jumanne Julai mosi mwaka huu, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Israel ilikuwa imekubaliana na masharti ya kusitisha mapigano kwa siku 60 wakati mauaji kwenye ukanda wa Gaza yakiwa kwenye mwezi wake wa 21.

Trump alidai kwamba Misri na Qatar, ambazo ni wapatanishi wakuu, walikabidhiwa jukumu la kuwafikishia mapendekezo hayo Hamas lakini wakati huo huo akilitishia kundi hilo kutokuutakaa mpango huo.

“Tunaamini kwamba Misri na Qatar wanaendelea na mpango mzuri wa upatanisho na suala hili linafaa kuchukuliwa kwa uzito zaidi lakini pia ni lazma Hamas iwe waangalifu na kuzingatia masharti hayo”, alisema Trump.

Baraza la usalama lajadili upatishi Gaza.

Waziri wa Mambo ya nje wa Israel, Gideon Saar, alisema sehemu kubwa ya mawaziri kwenye serikali ya nchi yake wanaunga mkono makubaliano hayo ambayo yanajumuisha kuachiliwa kwa mateka.

Waziri huyo wa mambo ya kigeni aliongeza kwamba sehemu kubwa ya raia wa Israel wanaunga mkono makubaliano hayo kama inavyothibitishwa na uchunguzi wa maoni.

Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatarajiwa kukutana na Rais Trump wiki ijayo mjini Washington, ili kuangazia zaidi mikakati na mipango ya kudhibiti.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

International News

Israel na Iran zakubaliana kusitisha mashambulizi

Published

on

By

Warning
Warning
Warning
Warning

Warning.

Makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Iran yameanza kutekelezwa huku nchi hizo mbili zikithibitisha tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu hatua hiyo.

Muda mfupi baada ya tangazo la Trump, taifa la Israel lilisema limeafikia malengo yake na ikathibitisha kwamba imesitisha mashambulizi, hatua iliyotafsiriwa kama mwisho wa vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi, ilikanusha kuwepo kwa makubaliano yoyote ya kusitisha mashambulizi, akisema kwamba Iran haina nia ya kuendeleza mashambulizi, lakini bado haijakubali rasmi kusitisha mapigano.

Licha ya kauli za kusitishwa kwa mashambulizi ya makombora kati ya nchi hizo mbili, Jeshi la Ulinzi la Israel limeripoti mashambulizi mapya yaliyotokea kutoka upande wa Iran.

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz alisema Iran ilikiuka usitishaji wa mapigano kwa kurusha makombora, akisema huenda jeshi la Israel likaanza tena kuishambulia Iran.

Iran ilikanusha habari kwamba imefanya mashambulizi ya makombora kuelekea Israel baada ya nchi hizo mbili kukubali kusitisha mapigano.

Mataifa mbalimbali ulimwenguni yamepongeza hatua ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Iran, huku taifa la China likizitaka nchini hizo mbili kutafuta suluhisho la kisiasa kwa mzozo kati yao.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending