Connect with us

News

Mung’aro: Miradi yote ya kaunti kukamilika 2026

Published

on

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amesema serikali yake iko mbioni kuhakikisha miradi yote ya maendeleo katika kaunti inakamilika kufikia mwezi juni mwaka ujao wa 2026.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi kwa makundi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo wanaoishi na ulemavu na wakongwe mjini Kilifi, gGavana Mung’aro alisema miongoni mwa miradi hiyo ni ufunguzi wa uwanja mpya wa michezo mjini Kilifi, uzinduzi wa makao makuu ya kaunti miongoni mwa miradi mingine.

Gavana Mung’aro pia alidokeza kuwa serikali yake inapanga kuanzisha ujenzi wa hospitali ya Ganze ambao utagharimu zaidi ya shilingi milioni 350.

Kiongozi huyo wa kaunti alisema ujenzi wa makao makuu ya kaunti unaendelea na utakapokamilika utarahisisha upatikanaji wa hudumua kwa wakaazi wa Kilifi vile vile kupunguza gharama ya matumizi ya fedha kwa kaunti.

“Kila mradi ambao tumeanza lazima ukamilike kufikia juni 2026, lazima tufungue makao makuu ya kaunti, lazima tufungue kiwanja chetu kipya cha mpira, lazima tufungue hospitali zetu za Mariakani, Kilifi, Bamba, pia tutaanza kujenga hospitali ya Ganze ya zaidi ya shilingi milioni 350”, alisema Mung’aro.

Wakati huo huo alishauri makundi yaliyopokezwa hundi hizo kuhakikisha wanazitumia kuekeza kwenye miradi ya maendeleo ili kuboresha maisha yao vile vile kunufaisha makundi mengine.

“Haya ndiyo mabadiliko tunayoyakusudia tulipoanzisha mfuko wa wezesha, hata hivyo uendelevu wa mfuko huu unategemea ulipaji wa mikopo kwa wakati, kila malipo yanaporejeshwa yanatuwezesha kufadhili makundi mengine yaliyotuma maombi, leo hii tunapozindua rasmi mpango huu wa uzima cash transfer ambao unalenga jamii zetu zisizojiweza hasa wazee katika wadi zote 35, tuko na watu 1,205 kila mmoja atapata shilingi 18,000 ambazo ni malimbikizi ya miezi tisa iliyopita.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending