County
Mung’aro Awaonya Madaktari na wahudumu wa Afya Wenye Hulka ya Kuiba Dawa Hospitalini

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amewaonya madaktari na wahudumu wengine wa afya katika kaunti hiyo wenye hulka ya kuiba madawa hospitalini, akisema kwamba watakaopatikana watakabiliwa kisheria.
Akizungumza baada ya kuzindua kitengo cha Radiolojia katika jengo la Kilifi County Medical Complex, Gavana Mung’aro amesema tangu aingie uongozini Serikali yake imefanikiwa kuwakamata wale ambao wamekuwa wakihusika na wizi wa madawa hospitalini.
Kiongozi huyo amesema serikali ya kaunti hiyo kwa ushirikiano na wadau wengine wanaendeleza mikakati ya kuhakikisha hospitali na zahanati za umma katika kaunti hiyo zinakuwa na vifaa vya kisasa vya matibabu.
“Nilipoingia kama Gavana nilianza kusafisha hii kaunti kwa sababu tulipokuwa walikuwa wengi sana lakini inakaa bado wako kwamba watu wanalipa pesa na watu wanapeleka pesa kwa akaunti zao ama wanatengezewa liseni bandia apewe na watu wachukue pesa waeke mfumo, nataka kuwahakikisha kwamba siku chache zijazo nitangaza watu wengi sana ambao wataenda nyumbani,” Gavana Mung’aro.
Kwa upande wake Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Chibule amesema ushirikiano zaidi utaendelezwa, kati ya serikali ya kaunti na wadau wengine ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa ipasavyo.
Ameahidi kumuunga mkono Gavana Mung’aro kufanikisha juhudi bora za utoaji wa huduma kwa wakaazi wa kaunti ya Kilifi, akisema hiyo ndio hatua pekee ya kuhakikisha wananchi wananufaika na miradi ya maendeleo.
“Sisi tuko nyuma yake kumuunga mkono na kwa yeyote yule ambaye ataingia kwa siasa hayo ni ya 2032 lakini tugange haya ya leo ya kwamba siku hii ya leo tunafurahikia tuna mashine ya kufanya ukaguzi wa kiafya,” Chibule.
County
Kilifi Imeweka Mikakati Bora ya Kuhakikisha Hospitali na Zahanati Zinakuwa na Madawa ya Kutosha

Naibu Gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule amesema serikali ya kaunti ya Kilifi imeweka mikakati bora ya kuhakikisha hospitali na zahanati zote za umma katika kaunti hiyo zinakuwa na madawa ya kutosha.
Chibule amesema tayari serikali ya kaunti hiyo imepitisha bajeti ya fedha za ziadi ili kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi mashinani, akiwarai wakaazi na wahudumu wa afya kuhakikisha wanalinda madawa hayo.
Akizungumza wakati wa zoezi la uzinduzi wa ujenzi wa jengo la Huduma Centre katika eneo bunge la Ganze, Chibule amesema sekta ya afya hadi mashinani itaboreshwa zaidi.
“Kuna mpango ambao tunaufanya ambao ni kuchukua madawa yetu kutoka KEMSA, japo ule mpango tulikuwa tunataka iko chini ya asilimia 20 lakini madawa yalifika. Nawahimiza wahudumu wa afya na wananchi kulinda raslimali zetu’, alisema Chibule.
Wakati uo huo amepongeza uzinduzi wa ujenzi wa jengo la huduma Centre katika eneo bunge la Ganze, akisema kwamba huduma zote za umma sasa itakuwa zinapatikana kwa urahisi hadi mashinani pindi ujenzi huo utakapokamilika.
County
Wakereketwa wa Siasa Magarini Walitaka Jopo la Uteuzi wa Makamishna Wapya wa IEBC Kukamilisha zoezi kwa Muda Unaofaa

Wakereketwa wa maswala ya kisiasa katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wamelitaka jopokazi la uteuzi wa Makamishna wapya wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kukamilisha kwa muda unaofaa uteuzi wa Makamishna hao.
Wakiongozwa na Emmanuel Ngumbao, wakereketwa hao wamesema hatua hiyo itasaidia kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Magarini kwani eneo bunge hilo limesalia bila ya mwakilishi bungeni.
Ngumbao amehoji kwamba eneo bunge hilo limekosa maendeleo kwa mda mrefu kutokana na Mahakama kuu kubatilisha uchaguzi wa Harrison Kombe aliyekuwa mbunge wa eneo hilo.
Wakati huo huo amesisitiza haja ya swala la uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Magarini kupewa kipaumbele baada ya kuapishwa kwa Makamishna wapya wa IEBC.