News
Mung’aro achaguliwa kuwa Mwenyekiti wa ODM kaunti ya Kilifi

Uchaguzi wa viongozi wa mashinani wa Chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi ulifanyika Agosti 25, 2025 licha ya awali kuhushudiwa vurugu baada ya kutofautiana kwa wafausi wa chama hicho.
Gavana wa kaunt ya Kilifi Gedion Mung’aro alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi na kuchakuwa nafasi ya Teddy Mwambire, baada ya kumbaduliwa uongozini kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.
Naibu Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi alichaguliwa Joseph Chilumo, Katibu mkuu akichaguliwa Ken Chonga ambaye ni mbunge wa Kilifi Kusini na Mwekahazina akachaguliwa Paul Katana ambaye ni Mbunge wa Kaloleni katika uchaguzi huo wa viongozi wa mashinani wa chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi.
Mengine waliochaguliwa ni pamoja na Tima Abuu, Abdallah Kombe, Caro Kalume, Mae Mwadena, Nickson Muramba, Harrison Kombe Twahir Abdul, Rashid Mohamed miongoni mwa viongozi wengine.
Vurugu hizo zilitokea wakati wasimamizi kwenye lango la ukumbi huo wanaoegemea mrengo wa Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro, walipodai kwamba baadhi ya wanachama sio wanachama halisi.
Wafuasi wa Mwakilishi wadi ya Ganda Oscar Wanje ambaye alikuwa anawania wadhifa wa uenyekiti wa vijana kaunti ya Kilifi alilazimika kujiondoa katika wadhfa huo kwani ni kati ya miongoni mwa wale waliozuiliwa kuingia katika ukumbi wa uchaguzi huo na nafasi hiyo ikachaguliwa Abdallah Kombe.
Wafuasi hao walikosoa utaratibu mzima wa maandalizi ya uchaguzi huo, wakishikilia kwamba watawasilisha malalamishi yao kwa kamati kuu ya uchaguzi ya chama cha ODM kupinga uchaguzi huo.
Wafuasi hao wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Ganze Karisa Ngirani, walilaumu utaratibu wa shughuli hiyo, wakisema umekosa kuzingatia haki ya wanachama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
Entertainment8 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment20 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News17 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni