Connect with us

News

Mudavadi: Uhusiano wa Kenya na Marekani uko imara

Published

on

Waziri wa Masuala ya kigeni Musalia Mudavadi amepuuzilia mbali madai kuwa uhusiano kati ya Kenya na Marekani unayumba.

Hii ni kufuatia mswada uliowasilishwa katika bunge la Congress na seneta James Risch wa Marekani.

Risch alipendekeza Kenya ipokonywe hadhi yake ya mshirika asiye mwanachama wa NATO akitaja hatua ya Kenya kujihusisha zaidi na Uchina.

Pendekezo lengine ni pamoja na tuhuma za Kenya kushirikiana na kundi la waasi wa RSF nchini Sudan.

Mudavadi alisisitiza mswada huo sio msimamo wa serikali ya Marekani, akishikilia kuwa uhusiano wa Nairobi na Washington unasalia imara.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending