News
Msithubutu Maandamano ya Sabasaba Mombasa – Polisi Yaonya

Idara ya Usalama mjini Mombasa imetoa taarifa kujibu ombi la wanaharakati wanaotaka kuandaa maandamano ya kuadhimisha siku ya SABA SABA mjini Mombasa.
Katika barua iliyotiwa Saini na Afisa mkuu wa Polisi (OCS) wa kituo Cha Central mjini Mombasa, Sylvester Wambua, ombi hilo limekataliwa kwa sababu za kiusalama, Polisi wakidai wana taarifa za kijasusi kwa maandamano hayo huenda yatatumiwa na wahuni kuvuruga amani, kusababisha maafa na uharibifu wa mali.
Ombi hilo liliwasilishwa na mwanaharakati Bradley Ouna. Maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika katika Barabara ya SABA SABA hadi Mwembe Tayari, mzunguko wa Fountanella na kuishia Uhuru gardens eneo la Mapembe ya Ndovu kwenye Barabara ya Moi Avenue.
Siku ya SABA SABA huadhimishwa kukumbuka harakati za ukombozi wa pili nchini Kenya ulitoa nafasi ya utawala wa Vyama vingi nchini .
Charles Rubia na Kenneth Matiba wakishirikiana na Jaramogi Oginga Odinga ni miongoni mwa viongozi waliowaongoza Genz wa miaka hiyo, kama vile James Orengo, Paul Muite na wengineo kumshurutisha Rais Daniel Arap Moi kuondolea mbali kifungu 2 A cha katiba ya Kenya, na kutoa nafasi ya siasa vya Vyama vingi nchini.
News
Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya TB

Kaunti ya Mombasa imetajwa miongoni mwa kaunti zinazoongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu eneo la pwani.
Everlyn Kibuchi mkurugenzi wa mradi wa kuhamasisha kuhusu ungojwa wa kifua kikuu unaofahakima kama Stop TB Project, alitaja mikusanyiko ya watu, ukosefu wa lishe bora na magonjwa ya kuambukiza miongoni mwa vinavyochangia maambukizi ya TB.
Akizungumza katika warsha iliyowaleta pamoja wanahabari jijini Mombasa, Kibuchi alisistiza umuhimu kwa jamii kufahamu dalili za maradhi ya kifua kikuu na kupata matibabu kwa wakati unaofaa.
“Mombasa ni eneo moja ambalo liko na janga kubwa sana la kifua kikuu nchini, changamoto ambayo inafanya kifua kikuu iwe shida zaidi hapa Mombasa ama pwani nimkwamba Tb inaenea zaidi mahali ambapo kuna mkusanyiko wa watu, kama mtu amepatikana na huo ugonjwa inafaa wale ambao wanaishi nayeye wao pia wanafaa wapimwe kwa sababu kunauwekano kuwa wameambukizwa”, alisema Kibuchi.
Mkurugeniz huyo vile vile alisema unyanyapaa miongoni mwa wanaoishi na ugonjwa wa kifua kikuu umechangia wengi kukosa kufanyiwa vipimo kwa hofu ya kupatikana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.
“Watu wanaogopa kwenda kupimwa kwa sababu wakoishi katika hali ya unyayapaa, wanmajishuku pengine wakipatikana na kifua kikuu watapatikana na maambukizi ya ukimwi, sio watu watote ambao wako na kifua kikuu wanaishi na ukimwi, ni asilimia 23 ya watu Kenya nzima ambao wako na kifua kikuu na ambao wako na ukimwi, hii inamaanisha asilimia 70 hawana virusi”, aliongeza Kibuchi
Kwa upande wake Deche Sanga afisa anayesimamia kitengo cha ugonjwa wa kifua kikuu katika kaunti ya Kilifi, aliweka wazi kwamba waraibu wa dawa za kulevya 5,000 kaunti ya Kilifi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi ya TB, japo wameweka mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.
“Kilifi tuko na takriban waru 5,000 wanaotumia dawa za kulevya, asimilia kubwa ya wanaoishi na TB wanaishi katika haya maeneo ambayo wanavuta unga, hii imefanya Kilifi tumekuja na mbinu ya kudhibiti hili tatizo, tumefungua vituo vya waraibu wa kurekebisha tabia tukishirikiana na wadau wengine, kwa mfano tuko na Omar project Malindi, malengo yake ni kupunguza madhara tukichanganya na HIV”, alisema Sanga.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Biwott: Polisi waendelea kuwasaka waumini wenye itikadi potovu

Kamanda wa Polisi kaunti ya Kilifi Josephat Biwott amepongeza juhudi za wakaazi wa kaunti hiyo kwa kuwa na ushirikiano mwema na asasi za usalama.
Biwott amesema ni kupitia ushirikiano huo ambapo oparesheni ya kuwanasa waumini wa dini potofu eneo la Binzaro, kilomita chache kutoka eneo la Shakahola imefanikiwa kutokana na juhudi za wakaazi kutoa taarifa kwa maafisa wa usalama.
Akizungumza na Coco Fm, Biwott alithibitisha kwamba eneo la Chakama lipo chini ya ulinzi wa polisi.
Biwott alidhitisha kuwa washukiwa 11 tayari wamekamatwa na wamefikishwa Mahakamani Jumanne 22 Julai 2025 mbele ya Hakimu Mwandamizi Joy Wesonga na wataendelea kuzuiliwa katika kituo cha Polisi mjini Malindi.
Biwott aidha alisema maafisa wa usalama wanachunguza iwapo washukiwa hao walienda msituni wakiwa na watoto.
“Nawashukuru wananchi wetu hasa wakaazi wa Binzaro, kwa kutueleza kwa mapema sana kuhusu yale mambo yalikua yanaendelea huko kwa vile wametueleza tumefaulu kuokoa wale ambao tumeokoa na wanaoendelea dini hiyo tumewakamata na wamefikishwa mahakamani”. …alisema Biwott, kwa njia ya simu.
Tarifa ya Elizabeth Mwende