Sports
Mshambulizi Wa Man.United Rashford Ni Mali Barca Ila Hataanza

Mshambulizi wa Manchester United Marcus Rashford akamilisha vipimo nchini Uhispania hapo jana.
Hata hivyo Baada ya Marcus Rashford kukamilisha vipimo hivyo vya afya kwa mafanikio huko Barcelona inaelezwa kuwa huenda asichezeshwe kwa mara ya kwanza kutokana na kutokuwa na utimamu wa kutosha wa mechi.
Rashford anatarajiwa kushiriki katika mazoezi yake ya kwanza akiwa na Barcelona hiyo hii leo ambapo mazoezi yake ya awali yataanza asubuhi na kuendelea hadi alasiri ili kumpa fursa ya kuhisi mazingira yake mapya.
Hafla rasmi ya kusaini mkataba imepangwa kufanyika kesho Julai 23 huko Spotify Camp Nou ambapo Rashford ataungana na Rais wa klabu ya Barcelona Joan Laporta.
Mwingereza huyo pia atazungumza na vyombo vya habari kwa mara ya kwanza akiwa mchezaji wa Barcelona baada ya uwasilishaji wake.
Mara tu kila kitu kitakapokamilika, Rashford anatazamiwa kusafiri na Barcelona kwa ziara yao ijayo ya Asia.
Mechi yake ya kwanza kwa kilabu inaweza kuja wakati wa mechi za kirafiki ingawa usawa wake wa mechi ndio utakaoamua kama atacheza mara moja ambapo Klabu itatathmini hali yake mazoezini kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho.
Chanzo: Mundo Deportivo
Continue Reading
Sports
Kocha Wa Stars Benni McCarthy Atoa Sababu Ya Kujiondoa CECAFA

Mkufunzi wa Timu ya Taifa ya Soka Harambee Stars Benni McCarthy amesema kwamba walienda Tanzania kushiriki Kombe la CECAFA wakiwa na azma na ari kubwa ya kuhahakisha wanajiandaa vyema kwa taji la Chan mwezi Ujao ila mandhari waliokutana nayo hayakua ya kuridhisha ndipo wakafikia makubaliano ya kurejea nchini.
Akizungumza kwa mara ya kwanza vijana wa nyumbani wakizidi kujinoa Ugani Nyayo mwalimu huyo amekiri mortisha iliku juu mno ila mazingira hayo hayangeruhusu wao kufanya Kazi na kujianda Ugani Karatu Arusha. “Tuliketi chini kama benchi la Kiufundi tukaona ubora wa viwanja vya mazoezi na wa michezo tukaona itakua si salama kwa wachezaji kuelekea CHAN hivyo tukarejea”.
Haya yanajiri baada ya stars kujiondoa kwenye kipute Cha CECAFA Cha Mataifa Manne nchini Tanzania siku ya Jumatatu huku maswali chungu nzima yakibaki vinywani mwa wengi.
Hata hivyo mwalimu huyo anasema kwa sasa wanajitayarisha zaidi kwa Kombe Hilo kwani wanajua fika ugumu wa kundi lao.
Stars wako KUNDI A pamoja na Angola, Morocco, Zambia na DR.Congo.
Sports
England Ndaani Ya Fainali EURO Ya Akina Dada

Mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la Mataifa ya Ulaya kwa Wanawake #WEURO Uingereza (England) wametinga fainali ya michuano hiyo kwa mwaka 2025, #WEURO2025 kufuatia ushindi wa 2-1 kwenye muda wa ziada wakiifunga Italia kwa mara ya kwanza kihistoria.
England imetangulia fainali kumsuburi mmoja kati ya Uhispania au Ujerumani watakaochuana hii leo kwenye nusu fainali nyingine ya #WEURO2025
FT: England 2-1 Italy
90+6′ Michelle Agyemang
119′ Chloe Kelly
33′ Barbara Bonansea