Connect with us

News

Msaidizi wa mbunge wa Kilifi Kusini afikishwa Mahakamani.

Published

on

Mahakama ya Shanzu, Kaunti ya Mombasa, imemuachilia kwa dhamana ya shilingi laki mbili au pesa taslimu ya shilingi laki moja msaidizi wa kibinafsi wa Mbunge wa Kilifi Kusini.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyowasilishwa mahakamani, mnamo Juni 3, mwaka 2024, katika eneo la Half London, Majengo, Kanamai, Kaunti ya Kilifi, Victor Katana Mganga pamoja na wenzake ambao hawakufika mahakamani, walidaiwa kushirikiana kubomoa ukuta kinyume cha sheria, mali ya Duncan Mkala Kumbe.

Aidha, Katana anakabiliwa na shtaka la pili ambapo inadaiwa kuwa mnamo Juni 21, mwaka 2024, katika eneo hilo hilo la Half London, Majengo, Kilifi Kusini, pamoja na washukiwa wengine ambao pia hawakuwa mahakamani, walishirikiana kubomoa ukuta mwingine wenye thamani ya shilingi milioni sita, mali ya Kassim Abdalla Mohammed.

Hata hivyo, Katana amekana mashtaka yote mawili dhidi yake.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending