Entertainment
“Mrs. Nasibu”: Zuchu Athibitisha Uhusiano Wake Rasmi na Diamond Platnumz?
Msanii Zuchu awasha moto mitandaoni baada ya kujiita “Mrs. Nasibu” kwenye Instagram. Je, hii ni ndoa rasmi na Diamond Platnumz au kiki ya muziki? Soma zaidi ujue ukweli nyuma ya uhusiano huu unaotikisa Bongo Fleva!

Katika kile kinachoonekana kuwa tangazo rasmi la mapenzi yao, msanii wa kike kutoka Tanzania, Zuchu, amewasha moto mpya mitandaoni baada ya kuhariri bio yake ya Instagram na kuandika maneno mafupi yenye uzito: “Mrs. Nasibu – Diamond Platnumz.”
Kwa mashabiki na wapenzi wa burudani, hatua hiyo huenda ikatfsiriwa kama uthibitisho wa wazi kuwa Zuchu sasa si tu mpenzi wa Diamond Platnumz, bali mke wake halali. Lakini je, huu ni mchezo wa mitandao au kweli ndoa imeshafungwa?
Ikumbukwe kuwa Diamond Platnumz alitupia picha mitandaoni zinazomuonesha akifunga ndoa ya mkeka na Zuchu akizua gumzo mitandaoni wengine wakimpa hongera kwa hatua hiyo kubwa ya maisha.
Zuchu na Diamond wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu. Zaidi ni kwamba, wawili hao wamekuwa wakihusishwa na taarifa za kutengana hata kabla ya kufunga ndoa. Kuonekana pamoja mara kwa mara, safari za kimahaba, picha za karibu na maelezo ya hisia kwenye nyimbo zao—vyote hivyo vimekuwa vikiongeza moto wa tetesi.
Na sasa, kwa kuandika “Mrs. Nasibu”, Zuchu ameongeza msumari wa mwisho kwenye jeneza la tetesi—akigeuza uvumi kuwa ujumbe rasmi kwa dunia.
Kwa tamaduni nyingi, hasa Afrika Mashariki, hatua ya mwanamke kujiita “Mrs.” huwa haichukuliwi kwa mzaha. Hii inaweza kumaanisha kuwa ndoa imeshafungwa, au kwamba mipango iko kwenye hatua za mwisho. Lakini kwa mastaa kama Diamond na Zuchu, ambao maisha yao ni hadharani, hatua ya kufanya kitu kikubwa kama harusi kimya kimya inaweza kuwa ya kimkakati au ya kulinda faragha yao.
Diamond amekuwa kwenye uhusiano na wanawake wengi mashuhuri, wakiwemo Wema Sepetu, Zari Hassan, Tanasha Donna, na wengineo. Lakini hakuna aliyeonekana kupata heshima ya “Mrs. Nasibu” kama Zuchu. Je, hii inamaanisha kuwa Zuchu ndiye aliyemshika Diamond kikamilifu?
Hadi sasa, mashabiki wamegawanyika—wapo wanaoshangilia, wakiona kama ni hatua ya kukomaa kwa Diamond, na wapo wanaodai huenda ni kiki tu ya kazi mpya au video inayokuja.
Ikiwa ni kweli kuwa Zuchu sasa ni “Mrs. Nasibu”, basi huu ni ukurasa mpya katika maisha ya Diamond—na pia ushindi wa kihisia kwa Zuchu. Lakini hadi sasa hakuna picha ya pete, harusi au tangazo rasmi kutoka kwa Diamond mwenyewe isipokuwa lile chapisho la harusi ya mkeka iliyoambatanishwa na maneno yaliyowaacha mashabiki njia panda. Na kama ni kweli wameoana, mbona Zuchu hajamfollow Chibu pale Instagram?
Tunabaki na swali moja: Je, tumsalimu Zuchu kama malkia wa WCB, au tusubiri arusi ya taifa?
Je, wewe unasemaje kuhusu hatua ya Zuchu? Unadhani ni kweli au kiki ya kimuziki?
Niachie maoni yako hapa chini! 👇
Entertainment
Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua
Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.
Kwenye Facebook, Yena, aliandika:
“We give God all the Glory. #Ametutendea”
Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨
🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”
Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.
👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)
Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!
💍 Safari ya Upendo Yao
Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!
Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:
“AMETUTENDEA!” 🎉
📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.
Entertainment
Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien
Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.
Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!
Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.
Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.
Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.
Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.
Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.
Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.