Connect with us

Entertainment

“Mrs. Nasibu”: Zuchu Athibitisha Uhusiano Wake Rasmi na Diamond Platnumz?

Msanii Zuchu awasha moto mitandaoni baada ya kujiita “Mrs. Nasibu” kwenye Instagram. Je, hii ni ndoa rasmi na Diamond Platnumz au kiki ya muziki? Soma zaidi ujue ukweli nyuma ya uhusiano huu unaotikisa Bongo Fleva!

Published

on

Katika kile kinachoonekana kuwa tangazo rasmi la mapenzi yao, msanii wa kike kutoka Tanzania, Zuchu, amewasha moto mpya mitandaoni baada ya kuhariri bio yake ya Instagram na kuandika maneno mafupi yenye uzito: “Mrs. Nasibu – Diamond Platnumz.”

Kwa mashabiki na wapenzi wa burudani, hatua hiyo  huenda ikatfsiriwa kama uthibitisho wa wazi kuwa Zuchu sasa si tu mpenzi wa Diamond Platnumz, bali mke wake halali. Lakini je, huu ni mchezo wa mitandao au kweli ndoa imeshafungwa?

Ikumbukwe kuwa Diamond Platnumz alitupia picha mitandaoni zinazomuonesha akifunga ndoa ya mkeka na Zuchu akizua gumzo mitandaoni wengine wakimpa hongera kwa hatua hiyo kubwa ya maisha.

Zuchu na Diamond wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu. Zaidi ni kwamba, wawili hao wamekuwa wakihusishwa na taarifa za kutengana hata kabla ya kufunga ndoa. Kuonekana pamoja mara kwa mara, safari za kimahaba, picha za karibu na maelezo ya hisia kwenye nyimbo zao—vyote hivyo vimekuwa vikiongeza moto wa tetesi.

Na sasa, kwa kuandika “Mrs. Nasibu”, Zuchu ameongeza msumari wa mwisho kwenye jeneza la tetesi—akigeuza uvumi kuwa ujumbe rasmi kwa dunia.

Kwa tamaduni nyingi, hasa Afrika Mashariki, hatua ya mwanamke kujiita “Mrs.” huwa haichukuliwi kwa mzaha. Hii inaweza kumaanisha kuwa ndoa imeshafungwa, au kwamba mipango iko kwenye hatua za mwisho. Lakini kwa mastaa kama Diamond na Zuchu, ambao maisha yao ni hadharani, hatua ya kufanya kitu kikubwa kama harusi kimya kimya inaweza kuwa ya kimkakati au ya kulinda faragha yao.

Diamond amekuwa kwenye uhusiano na wanawake wengi mashuhuri, wakiwemo Wema Sepetu, Zari Hassan, Tanasha Donna, na wengineo. Lakini hakuna aliyeonekana kupata heshima ya “Mrs. Nasibu” kama Zuchu. Je, hii inamaanisha kuwa Zuchu ndiye aliyemshika Diamond kikamilifu?

Hadi sasa, mashabiki wamegawanyika—wapo wanaoshangilia, wakiona kama ni hatua ya kukomaa kwa Diamond, na wapo wanaodai huenda ni kiki tu ya kazi mpya au video inayokuja.

Ikiwa ni kweli kuwa Zuchu sasa ni “Mrs. Nasibu”, basi huu ni ukurasa mpya katika maisha ya Diamond—na pia ushindi wa kihisia kwa Zuchu. Lakini hadi sasa hakuna picha ya pete, harusi au tangazo rasmi kutoka kwa Diamond mwenyewe isipokuwa lile chapisho la harusi ya mkeka iliyoambatanishwa na maneno yaliyowaacha mashabiki njia panda. Na kama ni kweli wameoana, mbona Zuchu hajamfollow Chibu pale Instagram?

Tunabaki na swali moja: Je, tumsalimu Zuchu kama malkia wa WCB, au tusubiri arusi ya taifa?

Je, wewe unasemaje kuhusu hatua ya Zuchu? Unadhani ni kweli au kiki ya kimuziki?
Niachie maoni yako hapa chini! 👇

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Published

on

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.

Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.

Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.

Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.

Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.

Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.

Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.

Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.

Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.

Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.

Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.

Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.

Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.

Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.

Chanzo: BBC

Continue Reading

Entertainment

Justin Bierber Arejea na Album Mpya ‘SWAGG’

Published

on

Msanii nyota wa muziki wa kimataifa, Justin Bieber, hatimaye ameachia rasmi albamu yake mpya na ya saba kwa jina “Swag”, ikiwa ni albamu yake ya kwanza tangu mwaka 2021 alipotoa Justice. Albamu hii imetoka leo na tayari imeanza kutikisa majukwaa mbalimbali ya muziki duniani.

Swag imejumuisha mastaa kadhaa akiwemo Gunna, Sexyy Red, Cash Cobain, pamoja na wasanii wengine wa kizazi kipya.

Albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 20 na tayari baadhi ya vibao kama “Go Baby”, “Soulful” na Butterflies “zimeanza kupokelewa vizuri kwenye mitandao ya Spotify, Apple Music na YouTube.

Hii ni mara ya kwanza kwa Bieber kuachia albamu tangu alipopata matatizo ya kiafya mwaka 2022 yaliyosababisha asitishe ziara yake ya kimataifa ya Justice World Tour ambayo ilikuwa iendelee hadi mwaka 2023.

Ziara hiyo ilisitishwa mnamo Septemba 2022 baada ya Bieber kupatwa na maradhi ya Ramsay Hunt Syndrome, ugonjwa uliomsababishia kupooza upande mmoja wa uso.

Kwa kipindi cha miaka minne bila kazi mpya, mashabiki wa Justin Bieber duniani wamekuwa wakimsubiria kwa hamu ujio wa kazi mpya kutoka kwake. Kupitia Swag, msanii huyo ameonyesha kurejea kwa nguvu na ubunifu wa hali ya juu, huku akiwa katika hali nzuri kiafya na kisaikolojia.

Taarifa na Francos Mzungu

Continue Reading

Trending