Connect with us

Entertainment

“Mrs. Nasibu”: Zuchu Athibitisha Uhusiano Wake Rasmi na Diamond Platnumz?

Msanii Zuchu awasha moto mitandaoni baada ya kujiita “Mrs. Nasibu” kwenye Instagram. Je, hii ni ndoa rasmi na Diamond Platnumz au kiki ya muziki? Soma zaidi ujue ukweli nyuma ya uhusiano huu unaotikisa Bongo Fleva!

Published

on

Katika kile kinachoonekana kuwa tangazo rasmi la mapenzi yao, msanii wa kike kutoka Tanzania, Zuchu, amewasha moto mpya mitandaoni baada ya kuhariri bio yake ya Instagram na kuandika maneno mafupi yenye uzito: “Mrs. Nasibu – Diamond Platnumz.”

Kwa mashabiki na wapenzi wa burudani, hatua hiyo  huenda ikatfsiriwa kama uthibitisho wa wazi kuwa Zuchu sasa si tu mpenzi wa Diamond Platnumz, bali mke wake halali. Lakini je, huu ni mchezo wa mitandao au kweli ndoa imeshafungwa?

Ikumbukwe kuwa Diamond Platnumz alitupia picha mitandaoni zinazomuonesha akifunga ndoa ya mkeka na Zuchu akizua gumzo mitandaoni wengine wakimpa hongera kwa hatua hiyo kubwa ya maisha.

Zuchu na Diamond wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu. Zaidi ni kwamba, wawili hao wamekuwa wakihusishwa na taarifa za kutengana hata kabla ya kufunga ndoa. Kuonekana pamoja mara kwa mara, safari za kimahaba, picha za karibu na maelezo ya hisia kwenye nyimbo zao—vyote hivyo vimekuwa vikiongeza moto wa tetesi.

Na sasa, kwa kuandika “Mrs. Nasibu”, Zuchu ameongeza msumari wa mwisho kwenye jeneza la tetesi—akigeuza uvumi kuwa ujumbe rasmi kwa dunia.

Kwa tamaduni nyingi, hasa Afrika Mashariki, hatua ya mwanamke kujiita “Mrs.” huwa haichukuliwi kwa mzaha. Hii inaweza kumaanisha kuwa ndoa imeshafungwa, au kwamba mipango iko kwenye hatua za mwisho. Lakini kwa mastaa kama Diamond na Zuchu, ambao maisha yao ni hadharani, hatua ya kufanya kitu kikubwa kama harusi kimya kimya inaweza kuwa ya kimkakati au ya kulinda faragha yao.

Diamond amekuwa kwenye uhusiano na wanawake wengi mashuhuri, wakiwemo Wema Sepetu, Zari Hassan, Tanasha Donna, na wengineo. Lakini hakuna aliyeonekana kupata heshima ya “Mrs. Nasibu” kama Zuchu. Je, hii inamaanisha kuwa Zuchu ndiye aliyemshika Diamond kikamilifu?

Hadi sasa, mashabiki wamegawanyika—wapo wanaoshangilia, wakiona kama ni hatua ya kukomaa kwa Diamond, na wapo wanaodai huenda ni kiki tu ya kazi mpya au video inayokuja.

Ikiwa ni kweli kuwa Zuchu sasa ni “Mrs. Nasibu”, basi huu ni ukurasa mpya katika maisha ya Diamond—na pia ushindi wa kihisia kwa Zuchu. Lakini hadi sasa hakuna picha ya pete, harusi au tangazo rasmi kutoka kwa Diamond mwenyewe isipokuwa lile chapisho la harusi ya mkeka iliyoambatanishwa na maneno yaliyowaacha mashabiki njia panda. Na kama ni kweli wameoana, mbona Zuchu hajamfollow Chibu pale Instagram?

Tunabaki na swali moja: Je, tumsalimu Zuchu kama malkia wa WCB, au tusubiri arusi ya taifa?

Je, wewe unasemaje kuhusu hatua ya Zuchu? Unadhani ni kweli au kiki ya kimuziki?
Niachie maoni yako hapa chini! 👇

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien

Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Published

on

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.

Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!

Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.

Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.

Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.

Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.

Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.

Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.

Continue Reading

Entertainment

#UlijanjarukaVipi! Safari ya Mpishi Nguli, Don Moses: Kutoka Kukosa Karo Hadi Kuwa Head Chef

Published

on

Katika dunia ya leo ambapo changamoto za kiuchumi zimewaacha vijana wengi wakihangaika, simulizi ya Don Moses ni mwanga wa matumaini kwa wengi.

Akiwa mgeni katika kipindi cha Janjaruka 254, kinachorushwa kila siku ya wiki kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, Moses alisimulia safari yake ya ajabu kutoka kwa kijana aliyezuiwa na karo ya shule hadi kuwa mpishi mashuhuri hadi kuwa Head Chef aliyesimamia wapishi waliosomea fani hiyo chuoni.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne, Moses alikuwa ameweka ndoto ya kujiunga na chuo lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti. Mama yake alipata ajali mbaya, hali iliyolazimu familia kuhamishia raslimali kwenye matibabu badala ya karo yake ya chuo.

“Nilijua wazi kuwa singeweza kulazimisha familia ichague kati ya maisha ya mama na elimu yangu. Ilibidi nitafute njia mbadala,” anasema Moses.

Jiko la YouTube: Darasa la Ukombozi

Akiwa hana karo, lakini akiwa na shauku, Moses alianza kujifunza sanaa ya upishi kupitia video za YouTube. Binamu yake, Moses Gambo, ndiye aliyemfungulia mlango wa maarifa kwa kumtambulisha kwenye tutorials mbalimbali mtandaoni.

Ni ujuzi huo wa mtandaoni uliomfungulia milango ya ajira katika hoteli za kifahari, ambapo aliweza kupanda ngazi hadi kuwa mpishi mkuu (Head Chef) — akiongoza wapishi waliopitia vyuo vya kitaaluma. Ni mafanikio ambayo wengi hawakuyatarajia kutoka kwa kijana ambaye hakuingia darasa la kawaida, bali alikaa mbele ya skrini.

“Najua kwenye upishi kuna kupika mashendea ama kupika chakula kibaya ila sijawahi kufeli. Siku zote mimi ni makini na ratio ya viungo. Ndiyo silaha yangu,” anasema kwa kujiamini.

Mwaka wa Mageuzi: 2020

Kama ilivyokuwa kwa wengi, mwaka wa janga la COVID-19 – 2020 – ndiyo ulikuwa mwaka wa mabadiliko makubwa kwa Moses. Akiwa na muda mwingi na motisha mpya, alianza kupika kibiashara, akihudumia watu waliokuwa majumbani.

“Kabula ya hapo, nilikuwa napika kwa kujifurahisha tu. Lakini corona ilinifungua macho. Nikaanza kuona kuwa mapishi ni biashara yenye nguvu,” anasema Moses.

Karo Iliyogeuka Mtaji

Kipindi fulani baadaye, Moses alipata nafasi ya kujiunga na chuo hatimaye. Lakini kwa mshangao wa wengi, alikataa ofa hiyo kwa hiari na kuomba fedha hizo zitumike kupanua biashara yake ya upishi.

“Nitamudu gharama ya chuo siku moja. Kwa sasa, najenga misingi. Muda wa kusoma utafika,” anasema.

💡 Ushauri kwa Vijana: Anza na Kile Kilicho Mkono Wako

Don Moses sasa ni sauti ya matumaini kwa vijana wengi wanaohisi kuwa elimu ya juu au mtaji mkubwa ndio tiketi pekee ya mafanikio. Anasisitiza umuhimu wa kuanza na huduma, si lazima mtaji.

“Kama huna kazi wala mtaji, toa huduma kwanza. Ukiwa na bidii na ubunifu, malipo yatafuata,” anashauri.

Leo hii, sehemu kubwa ya mapato ya Moses huingia moja kwa moja kwenye ununuzi wa vifaa bora vya upishi, huku akiendeleza ndoto yake ya kuwa mmoja wa wapishi wakubwa zaidi nchini Kenya.

Continue Reading

Trending