Connect with us

Business

Mradi wa kiuchumi wa Dongo Kundu wavutia wawekezaji zaidi

Published

on

Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaendelea kuonyesha nia ya kuekeza katika mradi wa kiuchumi wa dongo kundu kaunti ya Mombasa.

Mradi huo unaotarajiwa kuongeza uzalishaji katika viwanda na thamani ya bidhaa ndani ya nchi na nje, unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Kampuni ya nishati kutoka China, Ruike Energy Group Limited, ni mwekezaji wa hivi karibuni kuonyesha nia ya kupata nafasi ndani ya eneo hilo la kiuchumi la Dongo Kundu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta.

Kulingana na halmashauri ya bandari nchini KPA hatua hiyo italeta faida Zaidi ikiwemo kubuni nafasi za ajira, ikuaji wa uchumi, upatikanaji wa vifaa vya baharini, na urahisi wa kufikia masoko ya kanda na ya kimataifa.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KETRACO kuimarisha usalama wa chakula nchini

Published

on

By

Shirika la usambazaji umeme nchini, KETRACO, limethibitisha dhamira yake ya kuimarisha usalama wa chakula, ukuaji wa kijani, na ushirikiano wa kieneo kupitia uekezaji mkubwa katika miundombinu ya umeme.

Katika maonesho ya Kimataifa ya kilimo ASK yanayoendelea kaunti ya Mombasa, KETRACO imeonyesha jinsi miundombinu yake ya umeme inavyowezesha kilimo cha kisasa na uzalishaji wa viwandani.

Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi mkuu, mhandisi Kipkemoi Kibias, KETRACO imekamilisha miradi 43 ya njia za kusafirisha umeme, huku mingine 29 ikitarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2028.

Kibias, alisema shirika hilo tayari limejenga zaidi ya kilomita elfu sita za njia za umeme wa msongo mkubwa, likiwa pia na vituo 46 vya kusambaza umeme na upanuzi wa mitambo 33.

Katika eneo la Pwani, Kibias alisema upanuzi wa mpango wa Green Energy Backbone umewezesha usambazaji wa kawi safi kwa asilimia 93, jambo lililopunguza utegemezi wa mafuta na kuchochea maendeleo ya biashara za kilimo, utalii na uchumi wa baharini.

Kibias alisema KETRACO inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuunganisha Kenya na nchi jirani kupitia njia za kimataifa kama zile za Ethiopia, Tanzania na Uganda hatua zitakazowezesha biashara ya umeme Afrika Mashariki.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Muungano wa bodi za leseni za vileo wapinga sera ya NACADA

Published

on

By

Muungano wa bodi za kudhibiti na kutoa leseni za vileo nchini umepinga vikali pendekezo la Sera ya Mwaka 2025 ya Mamlaka ya Kudhibiti Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya (NACADA), wakidai kuwa linaenda kinyume na ugatuzi na kuondoa mamlaka ya kikatiba ya serikali za kaunti katika usimamizi wa biashara ya vileo.

Wakizungumza mjini Diani kaunti ya Kwale, wanachama wa Muungano huo wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Julius Owino, walisisitiza kuwa serikali za kaunti ndizo zenye jukumu la kisheria na kikatiba la kutoa leseni, kusimamia, na kutekeleza sheria zinazohusu uuzaji wa pombe.

“Sera hii ya NACADA ni jaribio la kuingilia majukumu ya kaunti na itaathiri mapato ya serikali za kaunti, kaunti lazima zisalie na mamlaka kamili ya kusimamia biashara ya vileo kama ilivyowekwa katika Katiba,” alisema Owino.

Owino pia aliitaka NACADA kushirikiana na kaunti kwa njia ya mashauriano badala ya kujaribu kuchukua majukumu yao, akiongeza kuwa ushirikiano thabiti ndio utaleta mafanikio katika udhibiti wa pombe na dawa za kulevya.

Kauli yake iliungwa mkono na Richard Osongo, Mwenyekiti wa wamiliki wa baa katika kaunti ya Kwale, ambaye alitoa onyo kali dhidi ya kile alichokiita “unyanyasaji wa mamlaka za kaunti na NACADA.”

Muungano huo ulieleza kuwa utatoa mapendekezo rasmi kwa serikali ya kitaifa na kuhimiza mjadala wa wazi kabla ya utekelezaji wowote wa sera hiyo mpya.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending