Connect with us

Sports

Morocco Waanza Mazoezi Nyayo Tayari Kwa CHAN

Published

on

SIKU 4 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN
Timu ya Taifa Ya Morocco marufu ‘Atlas Lions ‘ wamefanya mazoezi Yao ya kwanza Ugani Nyayo hapo jana kujinoa tayari kwa mechi ya ufunguzi.
Vijana hao waliwasili mapema Jana tayari kwa kipute hicho kinachongoa nanga Jumamosi hii ugani Benjamin Mkapa nchini Tanzania.
Badhi ya wachezaji nyota kwenye kikosi hicho ni pamoja na;mshambulizi El Mahraoui Anas pamoja na kiungo Khairi Ayoub wa RS Berkane.
Hii hapa ni kikosi chote cha Taifa hilo kwa kombe la CHAN;
Magolikipa:
  • Al Harrar Elmehdi
  • Rachid Ghanimi (FUS Rabat)
  • Aqzdaou Omar (Wydad Casablanca)

Mabeki:

  • Moufid Mohamed (Wydad Casablanca)
  • Boulacsout Mohamed
  • Mchakhchekh Mehdi
  • Louadni Marouane
  • Arrassi Bouchaib
  • Assal Abdelhak (RS Berkane)
  • Belammari Youssef (Raja Casablanca)
  • Zahouani Fouad

Viungo:

  • Khairi Ayoub (RS Berkane)
  • Hrimat Mohamed Rabie
  • Souane Amine
  • Essadak Houssam
  • Hajji Reda (RS Berkane)
  • Bach Anas
  • Aït Ouarkhane Khalid
  • Bougrine Sabir

Washambulizi:

  • Mehri Youssef (RS Berkane)
  • El Mahraoui Anass
  • Bouhra Saïf-Eddine (Wydad Casablanca)
  • Baba Khalid
  • Riahi Imad (RS Berkane)
  • Salaheddine Errahouli
  • Mouloua Ayoub
  • El Kaabi Youness
  • Lamlioui Oussama (RS Berkane) Morocco wanafungua kampeini Yao dhidi ya Angola siku ya Jumapili Ugani Nyayo kwenye kundi A.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Taifa Ya Nigeria Super Falcons Imepokea Zawadi Nono Kutoka Kwa Rais

Published

on

By

 Mabingwa wa Bara Afrika kwa soka la akina dada Super Falcons wamevuna vinono kutoka kwa rais wa taifa hilo punde tu baada ya kutua kutoka mjini Rabat Morocco.
Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu akitangaza zawadi zifuatazo kwa timu ya Super Falcons:
Kila mchezaji atapokea dola 100,000 za Kimarekani
Kila mchezaji atapewa nyumba ya vyumba vitatu
Kila mwanachama wa benchi la ufundi atapokea dola 50,000 za Kimarekani
Zaidi ya hayo, Jukwaa la Magavana wa Nigeria limewazawadia kila mchezaji kiasi cha ₦10 milioni (takriban dola 6,000 za Kimarekani).
Vipusa hao waliwashinda wenzao wa Morocco magoli 3-2 kwenye fainali kali iliosakatwa siku ya Jumamosi na kutwa ubingwa huo likiwa ni taji lao la kumi katika historia ya kombe hilo.
Continue Reading

Sports

Klabu ya KCB yatwaa ubingwa wa Raga ya Driftwood 7s mjini Mombasa

Published

on

By

Klabu ya KCB ndiyo mabingwa wa michuano ya Raga ya wachezaji saba kila upande ya Driftwood 7s iliyofanyika mjini Mombasa.

Hii ni baada ya kuibuka na ushindi wa alama 15–14 dhidi ya klabu ya Strathmore Leos katika fainali ya kusisimua iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mombasa Sports Club.

KCB, maarufu kama Mabenki, walianza mchezo kwa kasi na kutawala kipindi cha kwanza. Hata hivyo, Strathmore walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na walikuwa karibu kusawazisha, lakini walikosa kwa pointi moja pekee.

Katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu, Kabras RFC waliibuka na ushindi wa alama 21–10 dhidi ya Nakuru RFC, na hivyo kupanda kutoka nafasi ya nne waliyoshikilia mwaka 2024.

Wakati huo huo, katika Divisheni ya Pili, Zetech Oaks waliibuka kidedea kwa kuichapa NYS Spades kwa alama 10–0, na kutwaa ubingwa bila kuruhusu bao lolote.

Continue Reading

Trending