Connect with us

Entertainment

Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua

Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Published

on

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.

Kwenye Facebook, Yena, aliandika:

“We give God all the Glory. #Ametutendea”

Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨

🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”

Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.

👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)

Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!

💍 Safari ya Upendo Yao

Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!

Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:

“AMETUTENDEA!” 🎉


📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Published

on

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”

Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.

Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.

Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.

Continue Reading

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading

Trending