Connect with us

Entertainment

Millennials Bongo Tour: AY Kuwasha Moto Nairobi!

Published

on

Nguli wa Bongo Flava kutoka Tanzania, AY, ametua jijini Nairobi tayari kwa tamasha linalosubiriwa kwa hamu – Millennials Bongo Tour, litakalowasha moto Kilimani, Jumapili hii, tarehe 1 Juni.

AY ambaye hiyo jana ameachia vibao vipya SIMUONI na SI NDO MANAKE akishirisha na Harmonize na Darasa mtawalia, atakuwa sura ya tamasha hilo la kipekee la muziki wa Afrika Mashariki. Atasindikizwa na mwanamuziki mahiri kutoka Burundi, Kidum, pamoja na DJ Redbone wa Nairobi, anayejulikana kwa kuamsha burudani kwenye kila tamasha.

Tamasha hili linaahidi mchanganyiko wa kipekee wa vibao vya kumbukizi na ladha ya kisasa ya Bongo Flava. AY, anayejulikana kwa vibao vilivyotikisa chati kama Zigo, Touch Me Touch Me, na Microphone, amewaahidi mashabiki onyesho lisilosahaulika.

“Inahisi vizuri sana kurejea Nairobi. Nipo tayari kuwapa mashabiki wangu burudani ya kukumbukwa,” alisema AY mara baada ya kuwasili.

Kuongeza ladha ya kipekee, Kidum atapanda jukwaani na vibao vyake vya kuburudisha kama Mapenzi na Haturudi Nyuma, huku DJ Redbone akikoleza utamu kwa mchanganyiko mtamu wa Afrobeat, Bongo Flava, na nyimbo kali za ukanda huu.

Millennials Bongo Tour si tamasha la kawaida—ni sherehe ya kitamaduni inayotambua muziki wa Bongo kama daraja linalounganisha vizazi na mataifa. Toleo hili linatoa heshima kwa magwiji wa muziki wa Afrika Mashariki waliotengeneza historia na ambao wanaendelea kuwapa msukumo wasanii wapya hadi leo.

“Hili si tamasha tu—ni sherehe ya muziki wa Afrika Mashariki na fursa ya kipekee kwa mashabiki kuungana na magwiji waliounda sauti ya kizazi,” alisema mmoja wa waandaaji wa tamasha hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Published

on

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”

Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.

Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.

Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.

Continue Reading

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading

Trending