Connect with us

News

Miili mingine 4 yapatikana kwa Binzaro- Shakahola

Published

on

Mili mingine minne imepatikana ikiwa imeoza kiasi cha kutotambulika katika msitu wa Shakahola karibu na kijiji cha Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Mili hiyo ilipatikama na wenyeji waliokuwa wakiendelea na shughuli zao katika msitu huo ambao umegonga vichwa vya habari tangu sakata ya Mhubiri tata Paul Mackenzie.

Kupatikana kwa miili hiyo ilisababisha idadi ya maiti zilizopatikana katika kisha cha hivi punde kabisa cha mauaji kwenye kijiji cha Binzaro kufikia Miili minane.

Maafisa wa usalama wanatarajiwa kukusanya mabaki ya hayo ili kuyapeleka katika makafani ya hospitali ya Malindi ambako
miili mingine iliyopatiakana katika kisa cha kwanza cha mauaji ya Shakahola ‘One’ inahifadhiwa.

Majuma mawili yaliyopita, Maafisa wa Polisi walivamia msitu huo na kupata maiti nne na makaburi sita ambayo sasa yanasubiri kufukuliwa.

Wahusika waliokuwa wakiendesha mafunzo ya itikadi kali katika eneo hilo lenye vijumba vitamo, waliwahi kutoroka wakiacha maiti moja ambayo ilikuwa haijazikwa.

Shughuli za kufukua makaburi hayo bado haijafanyika huku eneo hilo la msitu wa Kwa Binzaro likiwekwa chini ya ulinzi wa maafisa wa usalama.

Msako dhidi ya maafisa hao bado unaendelea katika msitu huo wa Shakahola.

Mackenzie na wenzake 30 walikamatwa na sasa wanasubiri kukamilika kwa kesi yake inayoendeshwa katika Mahakama za mjini Mombasa.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending