Connect with us

News

Mgombea Urais 2027 Robert Watene Aahidi Kukabili Ufisadi

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 Robert Watene anasema taifa litanawiri zaidi na kuendelea iwapo wananchi watahakikishiwa usalama wa chakula.

Watene alisema swala hilo ni miongoni mwa mambo muhimu atakayoyapa kipambele katika manifesto yake.

Vile vile mgombea huyo alisema wananchi wanafaa kuhakikishiwa upatikanaji rahisi wa maji safi pamoja na mfumo bora wa huduma za afya kwa wote.

Alidokeza kuwa huduma za afya iwapo zitapelekwa karibu na wananchi, mambo mengi yataepukika ikiwepo gharama ya usafiri na mda kupotezwa miongoni mwa wananchi.

“Tuko na shida ya chakula cha tumbo na utaskia mara hakuna unga, hiki chakula tunataka tuangalie ni vipi tunaweza kuwezesha wakenya wote wawe wakipata chakula kila wakati, jambo la pili ni maji safi, unajua ni watu wangapi wanateseka na maji, kunawengine hata kupata hayo maji wameenda kilomita nyingi kupata maji, mabo ya matibabu tumeyafanya yawe magumu sana kwa wananchi wengi,na sio sawa, saa hii ukienda hapa hospitali kuu utapata foleni ndefu mtu anakwambia nimekuwa hapa siku mbili sijahudumiwa na daktari, mbona tufanye hivyo”,alisema Watene.

Wakati huo huo aliahidi kuangazia sekta ya elimu na kuifanya ya elimu iwe ya bila malipo nchini, kuboresha usalama wa nchi, kukabiliana na ufisadi pamoja na kutokomeza ukabila.

“Kuna mambo na masomo hatuko sawa hata kidogo, tunatakikana masomo yawe haki ya kila mtu, na kutoka gredi ya kwanza hadi chuo kikuu serikali igharamie hayo masomo, nafasi za kazi watu wengi hawana kazi ya kufanya na sio eti hawataki kufanya kazi, hakuna nafasi za kazi, kuna mnyama mmoja anaitwa ufisadi lakini napenda nimgawanye mara mbili, wakwanza anaitwa wizi wa mali ya umma, halafu mwengine ni mambo ya hongo na vitu vidogo vidogo, ukabila ni kitu kibaya sana unaweza fanya ujichukie, unawezafanya mpigane, muuane na tushaona yakifanyika, hii lazima tumalize”,alisistiza mgombe huyo.

Mwanaharakati huyo atakuwa miongoni mwa vigogo wa siasa ambao watapambana kwenye uchaguzi mkuu ujao ambapo kwa sasa baadhi yao wameanza kuuza sera zao kwa wakenya.

Taarifa na Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending