Connect with us

News

Mgombea Urais 2027 Robert Watene Aahidi Kukabili Ufisadi

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 Robert Watene anasema taifa litanawiri zaidi na kuendelea iwapo wananchi watahakikishiwa usalama wa chakula.

Watene alisema swala hilo ni miongoni mwa mambo muhimu atakayoyapa kipambele katika manifesto yake.

Vile vile mgombea huyo alisema wananchi wanafaa kuhakikishiwa upatikanaji rahisi wa maji safi pamoja na mfumo bora wa huduma za afya kwa wote.

Alidokeza kuwa huduma za afya iwapo zitapelekwa karibu na wananchi, mambo mengi yataepukika ikiwepo gharama ya usafiri na mda kupotezwa miongoni mwa wananchi.

“Tuko na shida ya chakula cha tumbo na utaskia mara hakuna unga, hiki chakula tunataka tuangalie ni vipi tunaweza kuwezesha wakenya wote wawe wakipata chakula kila wakati, jambo la pili ni maji safi, unajua ni watu wangapi wanateseka na maji, kunawengine hata kupata hayo maji wameenda kilomita nyingi kupata maji, mabo ya matibabu tumeyafanya yawe magumu sana kwa wananchi wengi,na sio sawa, saa hii ukienda hapa hospitali kuu utapata foleni ndefu mtu anakwambia nimekuwa hapa siku mbili sijahudumiwa na daktari, mbona tufanye hivyo”,alisema Watene.

Wakati huo huo aliahidi kuangazia sekta ya elimu na kuifanya ya elimu iwe ya bila malipo nchini, kuboresha usalama wa nchi, kukabiliana na ufisadi pamoja na kutokomeza ukabila.

“Kuna mambo na masomo hatuko sawa hata kidogo, tunatakikana masomo yawe haki ya kila mtu, na kutoka gredi ya kwanza hadi chuo kikuu serikali igharamie hayo masomo, nafasi za kazi watu wengi hawana kazi ya kufanya na sio eti hawataki kufanya kazi, hakuna nafasi za kazi, kuna mnyama mmoja anaitwa ufisadi lakini napenda nimgawanye mara mbili, wakwanza anaitwa wizi wa mali ya umma, halafu mwengine ni mambo ya hongo na vitu vidogo vidogo, ukabila ni kitu kibaya sana unaweza fanya ujichukie, unawezafanya mpigane, muuane na tushaona yakifanyika, hii lazima tumalize”,alisistiza mgombe huyo.

Mwanaharakati huyo atakuwa miongoni mwa vigogo wa siasa ambao watapambana kwenye uchaguzi mkuu ujao ambapo kwa sasa baadhi yao wameanza kuuza sera zao kwa wakenya.

Taarifa na Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mvuvi aliyezama baharini Watamu apatikana Tanariver

Published

on

By

Mwili wa mvuvi Hudhefa Laly aliyepotea baharini huko Watamu eneo bunge la Kilifi Kaskazini Kaunti ya Kilifi akiwa na ndugu yake Athman Laly umepatikana eneo la Shakiko -Mathole, kaunti ya Tana River.

Ndugu hao wawili walitoweka habarini siku ya Alhamisi 24, Julai 2025 katika bahari hindi wakati wakiendelea na shughuli zao za uvuvi.

Vitengo mbali mbali vya uokozi vimekuwa vikiendesha zoezi la kutafuta miili ya wawili hao kwa ushirikiano na wavuvi eneo la Watamu.

Kufikia sasa mwili wa Athman Laly kakake Hudhefa ungali haujapatikana huku juhudi za kuutafuta zikiendelea.

Jamii ya wavuvi katika eneo la Watamu ikiongozwa na kiongozi wa vijana Bakari Shaban iliiomba serikali ya kaunti ya Kilifi na ile ya kitaifa kununua boti za uokozi ili kusaidia kuokoa maisha wakati kunapotokea dharura baharini.

“Tunaomba tupate boti za kuokoa maisha baharini, popote alipo waziri Ali Joho angalau tupate boti za uokozi kama mbili hapa Watamu ni kitovu cha utalii kunamahoteli mengi, watalii wote wanaokuja Watamu mpaka leo hakuna boti za uokozi”, alisema Shaban.

Awali wao wazazi wa wavuvi waliopotea baharini Lali Athman Lali na Dhurai Mohamed Ali waliiomba serikali kuweka juhudi zaidi za kuwasaidia kuwapata wanawao kwani ndio tegemeo kubwa kwa familia yao.

“Uko usaidizi unatumika, kuna vijana wanaojitolea kwa maboti wanaenda ile sehemu ambayo wavuvi wanavua, wanajaribu kuzunguka lakini toka siku hiyo hawajapata chochote: Katika Maisha yangu mimi nawategemea hawa watoto kunisomeshea hawa watoto wangu ambao ni wadogo zao mashule, kwa chakula kwa hivyo naomba serikali inisaidie kwa sababu ndio tegemeo langu hao watoto”.walisema wazazi.

Kisa hiki kilijiri miezi kadhaa baada ya mvuvi mmoja kutoka eneo la Mnarani mjini Kilifi kufariki baharini baada ya kugongwa kichwani kwa pondo na wavuvi wenzake kulipotokea mzozo kuhusu pato la samaki.

Kufikia sasa mwili wa mvuvi huyo haujapatikana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya MPOX nchini

Published

on

By

Wizara ya afya nchini imesema kaunti ya Mombasa inaongoza kwa visa vya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa idara ya afya nchini Daktari Patrick Amoth, kaunti ya Mombasa imerekodi visa 139 kati ya visa 300 vilivyoripotiwa na wizara hiyo.

Amoth alidokeza kuwa serikali itatangaza siku maalum ya kutoa chanjo ya kudhibiti msambao wa ugonjwa huo wakishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO.

Mkurugenzi huyo vile vile alimesema zoezi hilo litaambatana na hamasa kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi zaidi.

“Kwa wakati huu Mombasa ndio inaongoza kwa idadi ya visa 139 kwa hivyo tuchuke tahadhari kuhakikisha kwamba tunazuia maambukizi, na tunafanya mpango pamoja na shirika la afya duniani WHO, hapa tutakuja na mpango wa chanjo na ikifika huo wakati tunaomba watu wajitokeze wapate chanjo ili wapate kinga”,alisema Daktari Amoth.

Wakati huo huo Amoth aliokeza kuwa uchunguzi wa vifo vya watu wanne walioaga dunia wiki chache zilizopita huko Migadini, eneo bunge la Changamwe kaunti ya Mombasa umebaini walifariki kutokana na magonjwa mengine na wala sio maambukizi ya ugonjwa wa MPOX kama ilivyodhaniwa na wakaazi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending