Connect with us

News

Mgombea Urais 2027 Robert Watene Aahidi Kukabili Ufisadi

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 Robert Watene anasema taifa litanawiri zaidi na kuendelea iwapo wananchi watahakikishiwa usalama wa chakula.

Watene alisema swala hilo ni miongoni mwa mambo muhimu atakayoyapa kipambele katika manifesto yake.

Vile vile mgombea huyo alisema wananchi wanafaa kuhakikishiwa upatikanaji rahisi wa maji safi pamoja na mfumo bora wa huduma za afya kwa wote.

Alidokeza kuwa huduma za afya iwapo zitapelekwa karibu na wananchi, mambo mengi yataepukika ikiwepo gharama ya usafiri na mda kupotezwa miongoni mwa wananchi.

“Tuko na shida ya chakula cha tumbo na utaskia mara hakuna unga, hiki chakula tunataka tuangalie ni vipi tunaweza kuwezesha wakenya wote wawe wakipata chakula kila wakati, jambo la pili ni maji safi, unajua ni watu wangapi wanateseka na maji, kunawengine hata kupata hayo maji wameenda kilomita nyingi kupata maji, mabo ya matibabu tumeyafanya yawe magumu sana kwa wananchi wengi,na sio sawa, saa hii ukienda hapa hospitali kuu utapata foleni ndefu mtu anakwambia nimekuwa hapa siku mbili sijahudumiwa na daktari, mbona tufanye hivyo”,alisema Watene.

Wakati huo huo aliahidi kuangazia sekta ya elimu na kuifanya ya elimu iwe ya bila malipo nchini, kuboresha usalama wa nchi, kukabiliana na ufisadi pamoja na kutokomeza ukabila.

“Kuna mambo na masomo hatuko sawa hata kidogo, tunatakikana masomo yawe haki ya kila mtu, na kutoka gredi ya kwanza hadi chuo kikuu serikali igharamie hayo masomo, nafasi za kazi watu wengi hawana kazi ya kufanya na sio eti hawataki kufanya kazi, hakuna nafasi za kazi, kuna mnyama mmoja anaitwa ufisadi lakini napenda nimgawanye mara mbili, wakwanza anaitwa wizi wa mali ya umma, halafu mwengine ni mambo ya hongo na vitu vidogo vidogo, ukabila ni kitu kibaya sana unaweza fanya ujichukie, unawezafanya mpigane, muuane na tushaona yakifanyika, hii lazima tumalize”,alisistiza mgombe huyo.

Mwanaharakati huyo atakuwa miongoni mwa vigogo wa siasa ambao watapambana kwenye uchaguzi mkuu ujao ambapo kwa sasa baadhi yao wameanza kuuza sera zao kwa wakenya.

Taarifa na Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mwanaharakati Mwabili Mwagodi apatikana

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Mwabili Mwagodi ambaye alidaiwa kutekwa nyara akiwa nchini Tanzania sasa amepatikana.

Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za kibinamu nchini la VOCAL Africa Hussein Khalid, alisema Mwabili alipatikana katika msitu wa Kinondo eneo bunge la Msambweni kaunti ya Kwale mwendo wa saa tisa usiku akitembea kuelekea Diani.

Khalid alisema Mwabili, anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya mjini Mombasa kisha baadaye atasafirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi kuungana na familia yake.

“Tunashukuru Mwabili amepatikana akiwa hai japo amedhohofika na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya na kisha atarudi Nairobi kukutana na familia yake lakini tunaiambia serikali ya Kenya na Tanzania ni lazima wahusika kukomesha tabia hii ya kuwateka watu nyara kuna sheria kama mtu amekosea apelekwe Mahakamani”, alisema Khalid.

Hata hivyo Wanaharakati hao wa kutetea haki za kibinadamu waliishtumu serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuwanyanyasa wanaharakati wa kijamii wa taifa la Tanzania na wale wanaoingia Tanzania kutoka mataifa mengine ili kuendeleza hamasa za haki za kijamii.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Herman yahairishwa

Published

on

By

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara ambaye ni raia wa Uholanzi, Rowenhorst Herman na mlinzi wake Evans Bokoro imeahirishwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu kufuatia Mahakama kuingia kwenye mapumziko rasmi ya majaji.

Mke wa Marehemu, Riziki Cherono pamoja na mshukiwa mwenza Timothy Omondi wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga na kutekeleza mauaji hayo yaliyotokea Juni 4 mwaka 2021 katika eneo la Shanzu kaunti ya Mombasa.

Katika kikao cha awali cha Mahakama, Afisa wa Polisi Koplo Richard Cheruiyot alieleza mbele ya Jaji Wendy Micheni kwamba Cherono alijaribu kuonekana kama mwathirika kwa madai ya kutekwa nyara na majambazi waliodaiwa kuvamia nyumba yao.

Afisa huyo alieleza kwamba walimkuta Cherono akiwa amefungwa kwenye usukani wa gari lake, huku akidai kwamba alivamiwa na kulazimishwa kuondoka nyumbani kwao akiwa chini ya tishio la bunduki.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa ulibaini kwamba Marehemu Herman alipatikana amefariki nyumbani kwake akiwa amefungwa mikono na miguu huku mlinzi wao, Evans Bokoro, alikutwa akiwa hai kwa taabu karibu na bwawa la kuogelea lakini baadaye alifariki akipelekwa hospitalini.

Mashahidi wa upande wa mashtaka pamoja na polisi, wanaamini kwamba Cherono ndiye mshukiwa mkuu wakidai kwamba alipanga na kufanikisha mauaji hayo kwa kushirikiana na watu wengine, wakiwemo waliotajwa kuwa sehemu ya genge lililovamia nyumba hiyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending