Connect with us

Business

Mataifa yanayoshuhudia ghasia yaibua wasiwasi wa usafiri wa ndege

Published

on

Kenya inapolenga kuongeza ushuru unaokusanywa katika sekta ya uchukuzi wa angani, suala la usalama wa ndege zinazosafiri kupitia mataifa yanayoshuhudia ghasia limeibua wasiwasi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya safari za ndege nchini Mary Keter alisema mabadiliko ya sera yanahitajika ili kupatia kipaumbele suala la ukaguzi na utathmini wa hatari zilizopo ili kuhakikisha ustawi hauathiri usalama au uendeshaji wa biashara.

Ikumbukwe kwamba shughuli za uchukuzi wa abiria humu nchini ziliongezeka kwa asilimia 38.5 mwaka uliopita huku wasafiri zaidi ya milioni 10 wakitumia uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta.

Haya yanajiri huku mikakati zaidi ikiendelezwa naMamlaka hiyo kuhakikisha uchukuzi wa angani unaimarika kwa asilimia kubwa licha ya changamoto za kiuchumi zinazolikumba taifa hili.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wahudumu wa Uchukuzi Kilifi Walia na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Published

on

Siku moja baada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini, EPPRA kutangaza kupandishwa kwa bei ya mafuta, sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Kilifi inaelezea hofu ya kuathirika kwa biashara zao.

Wahudumu wa tuktuk,teksi, bodaboda na magari ya usafiri wa umma hapa mjini Kilifi wanasema kupanda kwa bei ya petrol na diseli kutaathiri pakubwa sekta hiyo ya uchukuzi.

Sasa wanasema kuwa watalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na gharama ya mafuta.

Ni hali ambayo imeathiri wakaazi ambao wanatarajiwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri wakisema kuwa watalazimika kutembea kwa mguu kwa safari fupi fupi katika utekelezaji wa shughuli zao za kawaida.

Hatahivyo wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa inaingilia kati ili kuona kwamba bei za mafuta zinadhibitiwa.

Haya yamejiri huku lita moja ya mafuta aina ya petrol kaunti ya KIlifi ikiuzwa kwa shilingi 183.88 huku diseli ikiuzwa kwa shilingi 169.16 kila lita.
Lita moja ya mafuta ya taa inauzwa kwa shilingi 153.29.

Continue Reading

Business

Uhusiano wa Kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa Waonyesha Ukuaji Chanya

Published

on

Takwimu za kibiashara kati ya kenya na ufaransa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka 2024 zinaonyesha kuwa ufaransa ilileta humu nchini bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 6.5 na kuagiza bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 5.7 kutoka humu nchini hali iliyoleta uwiano bora wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili.

Nchi hiyo sasa inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na kenya ambapo kenya imewaalika waekezaji zaidi kutoka nchini ufaransa kuekeza katika sekta kadhaa za kenya.

Waziri mwenye mamlaka makuu Msalia Mdavadi anasema ufaransa inalenga sekta za kawi, miundomsingi na tekinolojia ili kuongeza biashara kati yake na kenya.

Continue Reading

Trending