Sports
Mashindano Ya Dunia Ya Handiboli Ya Ufukweni Kuanza Rasmi Tunisia

Kikosi cha Taifa mchezo wa Handiboli wachezaji chipukizi kuanza rasmi mashindano ya kombe la dunia hapo kesho mjini Tunis Tunisia.
Kulingana na droo iliyofanywa hii leo ni kwamba timu zote mbili upande wa wanaume na akina dada zimejumuishwa kundi B huku kikosi cha akina dada ikiratibiwa kumenyana na mataifa ya Uholanzi,Ujerumani,Rep of China kunid A zina timu za Ufaransa,Brazil,Thailand na Tanzania.
Kundi C zina timu za Tunisia,Hungary,Mexico na Senegal, Kundi la mwisho kundi D zina timu za Croatia,Uruaguay,Uhispania na Bulgaria.
Upande wa wanaume Kenya itamenyana na Hungary,Ujerumani na Tanzania huku kundi A likiwa na timu za Iran,Uhispania,Oman na Puerto Rico,Kundi C linajumuisha timu za Tunisia,Thailand,Mexico na Cook Island huku kundi D likiwa na timu Argetina,Brazil,Uruguay na Senegal.
Mashindano hayo yanaanza kesho na kukamilika Juni 22.
Sports
Fikirini Jacobs- Benni Mccarthy Ni Sahihi Harambee Stars

Katibu katika Wizara Kuu ya Kitaifa Inayosimamia Maswala ya Vijana na Uchumi Bunifu Fikirini Jacobs amesifia hatua ya Shirikisho la soka nchini FKF na serikali kupitia kwa Wizara ya Michezo kumteua Benni Mccarthy kuwa kocha mkuu wa timu ya soka wanaume Harambee Stars.
Kwa mujibu wa Katibu huyo hatua hiyo ni ishara tosha ya kufufuka kwa mchezo huo nchini baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye timu hiyo.
“Nichukue Fursa Hii kuwapongeza Wizara ya Michezo ambapo yuko mwenzangu Elijah Mwangi sitaki nizungumz mengi lakini hata hatua ya Taifa La Kenya kumchukua Benni Mccarthy aliyekua kocha Manchester United kuwa kocha wa Harambee Stars ni hatua ya kufufua timu hiyo pamoja na The Lost Glory ,kwa sababu kihistoria mimi ni mtu nimekaa na watu wengi akiwemo mzee wetu The RT HON.Raila Amollo Odinga na aliwahi kuniambia hapa kenya mpira ulikua mkubwa mno kuliko magharibi na hata Afrika Kusini.”
Katibu huyo aliyasema hayo katika fainali ya mashindano ya kaunti ya shule za Upili katika shule ya Upili ya kilifi towship.
Sports
Mchezaji Tenesi Alcaraz Bingwa Tena

Mchezaji Tenesi anayeorodheshwa wa Pili duniani kwa sasa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ameweza kuandikisha rekodi mpya baada ya kushinda taji la pili kombe la Queens Cup Title baada ya kumlaza Jiri Licheka raia wa Czech kwa seti za 7-5, 6-7 (5/7), 6-2 kabila ya finali ya Wimblendon.
Nyota huyo raia wa Uhispania alimzidi mwenzake kwenye fainali baada ya kuonyesha makali tokea mwanzo huku mchezaji huyo anayeorodheshwa wa 30 akikubali kichapo hicho kwa muda lisali 2 na dakika 10.
Mwanatenesi huyo tayari ana mataji matano baada ya kuzishinda fainali za French Open,Rome Open,Monte Carlo na Rotherdam mwaka huu wa 2025.
Mwamba huyo hajapoteza katika mashindano fainali 18 mpaka sasa tangu fainali za Barcelona Open April 20.
Titus Kesekwa
June 16, 2025 at 4:55 pm
Kazi safi sana kaka na Coco tv/radio.