Connect with us

News

Maseneta wamtaka Murkomen na Kanja kujiuzulu

Published

on

Maseneta katika bunge la Seneti wamemtaka Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen na Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja kueleza kilichosababisha kifo cha mwanablogu Albert Ojwang aliyefariki katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi.

Wamemtaka Murkomen kueleza umma kwa nini taarifa zilizotolewa na Kanja kuhusu kisa hicho zinakinzana na ripoti iliyotolewa na mwanapatholojia wa serikali Benard Midia baada ya kuufanyia upasuaji mwili wa Ojwang.

Akichangia hoja hiyo katika vikao vya bunge la Seneti, Seneta wa Kakamega Boni Khalwale amemtaka Waziri Murkomen kujiuzulu akidai kwamba amezembea katika utendakazi wake huku akimtaka Inspekta Kanja kuwaomba wakenya msamaha sawa na familia ya Ojwang’ haki inapatikana.

“Bwana Spika wazalendo wa nchi hii walipigana dhidi ya kuwekwa kizuizini bila kufunguliwa mashtaka na Waziri Murkomen ninakuhakikishia kwamba watapigana dhidi ya mauaji ya kiholela hasa wakiwa chini ya ulinzi wa polisi. heshima ya kijana huyu tafadhali wewe bado hujakuza mtoto hadi umri wa miaka 31, tafadhali si ya kibinafsi unaweza kujiuzulu mara moja kwani umeonyesha wazi haufai kushikilia wadhfa huo”, alisema Seneta Boni Khalwale.

Vikao hivyo hata hivyo vimeibua maswali mengi kuhusu mauaji ya kiholela na utekaji nyara nchini.

Taarifa ya Elizebeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Familia ya jamaa aliyezama baharini inalilia haki

Published

on

By

Familia ya Mwanamme aliyezama baharini katika kaunti ya Kilifi siku kadhaa zilizopita, inahimiza serikali kuongeza juhudi na kuwapa msaada wa kumtafuta jamaa wao.

Ikiongozwa na Omar Ali Omar ambaye ni Kakake Marehemu, Familia hiyo ilisema wamekuwa na wakati mgumu wa kuelekea baharini kila siku kwani kufikia sasa ni siku ya nne tangu jamaa wao azame baharini.

Aidha aliitaka serikali ya kaunti kutoa taarifa sehemu mbalimbali zinazopakana na ufuo wa bahari kwani huenda mwili wa Marehemu ukasukumwa na mawimbi hadi ufuoni. 

Familia ya jamaa aliyezama maji inalilia haki

Omar aliitaka idara ya kukabiliana na majanga katika kaunti kushirikiana na wavuvi wengine eneo la Mnarani pamoja na kutuma maboti zaidi kwa ajili ya uokozi wa mwili wa jamaa huyo kwani wamelazimika kugharamikia mafuta ya boti za ziada.

“Rescu timu ni boti moja, hiyo pekee yake kutafuta mtu kwa bahari ni vigumu vyombo vinatakikana vitoke vingi,washirikiene na sisi familia tuwekuongeza vyombo vya baharini kutafuta jamaa wetu, kwa sasa tunagharimika sasa boti kwenda baharini asubuhi na jioni inatugharimu shilingi elfu 16 kwa siku”, alisema Omar.

Kauli ya Omar imeungwa mkono na Mamake Marehemu ambaye ameshinikiza serikali ya kaunti kuingilia kati na kuhakikisha mwili wa mwanawe unapatikana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Nassir: Kaunti ya Mombasa wametenga milioni 80 za Afya

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Mombasa, Abdulswamad Shariff Nassir amesema serikali ya kaunti ya Mombasa wametenga shilingi milioni 80 kugharamia sehemu ya matibabu ya wakaazi ambao hutibiwa katika hospitali za Level 4 na Level 5.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa, Nassir alisema fedha hizo zitagharamia bima ya afya ya SHA ya wenyeji wa kaunti hiyo kwa muda wa mwaka mmoja.

Gavana Nassir pia alisema fedha hizo zitagharamia madeni ya ziada ya matibabu kwa watoto wa chini ya umri wa miaka 5 ambao wanatibiwa kupitia bima hiyo ya SHA.

“Tumeweka dawati maalum na fedha kuweza kuwalipia ile amana ambayo ilikuwa inalipiwa SHA. Na itakuwa sio ya Public health pekee lakini kando na Public health mnakuwa mumelipiwa kwa mwaka mzima’’, alisema gavana Nassir

Wakati huo huo Gavana Nassir alieleza matumaini kwamba mpango huo utasaidia kwa asilimia kubwa kuimarisha huduma za matibabu kwa wenyeji wa kaunti hiyo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending