News
Maseneta wamtaka Murkomen na Kanja kujiuzulu

Maseneta katika bunge la Seneti wamemtaka Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen na Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja kueleza kilichosababisha kifo cha mwanablogu Albert Ojwang aliyefariki katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi.
Wamemtaka Murkomen kueleza umma kwa nini taarifa zilizotolewa na Kanja kuhusu kisa hicho zinakinzana na ripoti iliyotolewa na mwanapatholojia wa serikali Benard Midia baada ya kuufanyia upasuaji mwili wa Ojwang.
Akichangia hoja hiyo katika vikao vya bunge la Seneti, Seneta wa Kakamega Boni Khalwale amemtaka Waziri Murkomen kujiuzulu akidai kwamba amezembea katika utendakazi wake huku akimtaka Inspekta Kanja kuwaomba wakenya msamaha sawa na familia ya Ojwang’ haki inapatikana.
“Bwana Spika wazalendo wa nchi hii walipigana dhidi ya kuwekwa kizuizini bila kufunguliwa mashtaka na Waziri Murkomen ninakuhakikishia kwamba watapigana dhidi ya mauaji ya kiholela hasa wakiwa chini ya ulinzi wa polisi. heshima ya kijana huyu tafadhali wewe bado hujakuza mtoto hadi umri wa miaka 31, tafadhali si ya kibinafsi unaweza kujiuzulu mara moja kwani umeonyesha wazi haufai kushikilia wadhfa huo”, alisema Seneta Boni Khalwale.
Vikao hivyo hata hivyo vimeibua maswali mengi kuhusu mauaji ya kiholela na utekaji nyara nchini.
Taarifa ya Elizebeth Mwende
News
Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.
Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.
“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi
Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.
Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira