Connect with us

News

Marekani yarusha makombora Iran, Trump akionya Tehran

Published

on

Marekani imerusha mabomu kwenye maeneo ya Vinu vya Nyuklia vya Iran yanavyojumuisha Fordo na kuharibu kabisa maeneo hayo hatua ambayo huenda ikachangia vita zaidi ya kimataifa.

Rais wa Marekani Donald Trump alisema maeneo hayo yanayojumuisha Fordo, yalipigwa na makombora ya jeshi la Marekani huku Marekani ikijiunga na mashambulio ya Israel dhidi ya mpango wa Nyuklia wa Tehran.

Katika hatuba yake vya vyombo vya habari, Rais Trump alisema kwamba ni lazima Iran isitishe vita na kukumbatia amani iwapo wanataka vinu vyao vya Nyuklia kutorushiwa makombora.

Picha kwa hisani

“Tayari tumevuruga na kuharibu vinu vya Nyuklia vya Iran na bado tutaendelea kurusha makombora ya kasi zaidi na kuharibu vinu vyote vya Nyuklia vya Iran iwapo makao ya Tehran hayatasalimu amri”, alisema Rais Trump katika hotuba yake.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi alilaani vikali shambulizi la Marekani na kusema kwamba ni shambulizi la kuchukiza na kwamba Tehran ina njia zote za kutetea uhuru wake.

“Matukio ya asubuhi ya leo ni ya kuchukiza na yatakuwa na matokeo ya milele. Kila Mwanachama wa Umoja wa Mataifa ni lazima ashtushwe na tabia hii hatari sana, isiyo ya kisheria bali ni tabia ya kihalifu,” alisema Seyed.

Seyed aliongeza kwamba Marekani ilifanya ukiukaji mkubwa wa Katiba ya Umoja wa Mataifa kama Mwanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho atangaza kuwania urais siku zijazo

Published

on

By

Waziri wa madini na masuala ya bahari nchini Hassan Ali Joho, alidokeza kwamba katika siku zijazo eneo la Pwani litatoa rais wa taifa la Kenya.

Waziri Joho aliwataka wakaazi wa Pwani kutojiingiza katika mivutano ya kisiasa na mirengo mingine ya kisiasa nchini, akisema ni wakati mwafaka wa wapwani kuungana na kujipanga kisiasa.

Waziri Joho alisema mtu ambaye alikuwa na nafasi nzuri ya kushikilia wadhfa huo wa kitaifa aliyekuwa ni Marehemu Karisa Maitha lakini ndoto hiyo bado ipo, akiweka wazi kwamba anamezea mate kiti hicho katika siku zijazo.

“Mara ya kwanza nilifikia kama kuna mpwani anaweza kuwa rais ilikuwa ni marehemu Karisa, lakini mimi hiyo ndoto bado niko nayo na nina imani iko siku bado hapa Pwani kuzaa rais. Siku moja wataskia rais Hassan na nikujipanga”, alisema Joho.

Joho alisisitiza haja ya wapwani kujipanga kisiasa ili kuwa katika nafasi nzuri ya kuvuna kwenye ngazi ya kitaifa pamoja na kuwa rahisi kwa eneo la Pwani kuwania kiti hicho na kutangaza rais wa Kenya katika siku zijazo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Waziri Joho na Mvurya waonya wanyakuzi wa ardhi.

Published

on

By

Waziri wa madini na uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho alisema serikali haitaruhusu tena wakaazi kufurushwa katika ardhi wanayoishi.

Akizungumza katika maeneo ya Mzambarauni mjini Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, Joho alionya kwamba mabwenyenye wenye hulka ya kufurusha wananchi kwenye ardhi za umma kamwe hawataruhusiwa.

Joho alisema wananchi hawafai kuhangaishwa kwenye ardhi zao huku akiwatahadharisha maafisa wa serikali dhidi ya kushirikiana na mabwenyenye kuhangaisha raia kwenye ardhi zao.

Hii ni baada ya kuibuka malalamishi ya mabwenyenye kutaka kuwafurusha wakaazi wa Utange Kaunti ya Mombasa.

Kwa upande wake Waziri wa michezo na Sanaa nchini Salim Mvurya alidokeza kuwa serikali inapanga kununua mashamba ambayo hayatumiki ili kuyakabidhi ya wananchi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending