Connect with us

News

Manchester United Ndaani Ya Fainali Europa

Published

on

Miamba wa Uingereza kilabu ya Manchester United imetinga kwenye fainali ya Europa ligi msimu huu kishindo bila kupoteza hata mechi moja.

Haya yanajiri baada ya vijana wa Kocha Ruben Amorim kuinyuka kabla ya kutandika sawa sawa kilabu ya Athletico Bilbao kichapo cha magoli 4-1 na jumla ya magoli 7-1

Wageni walichukua uongozi wa mapema kupitia kiungo Mikel Juregizer dakika ya 31 kipindi cha kwanza ,hata hivyo mashetani wekundu hao walirejea kwa moto wa radi kipindi cha pili wakijipatia magoli yao kupitia kiungo muingereza Mason Mount dakika ya 71 kabila ya Kiungo Casemiro kuongeza la pili dakika ya 80 huku mshmabulizi Rasmus Hojlund akicheka na nyavu dakika ya 85 na Mount Kuongeza lake la Pili na la nne kwa United dakika ya 93.

Katika matokeo mengine Tottenham Hotspurs walinyuka Bodo/Glimt 2-0 na jumla ya magoli 5-1 na sasa fainali ni kati ya timu za Manchester United na Spurs Ugani San Mames Uhispania Mei 21.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending