Connect with us

News

Mambo Atakia Kheri Rising Stars Misri Afcon u20

Published

on

Kiungo wa zamani timu ya taifa ya soka Harambee Stars Robert Mambo ametakia vijana wa timu chipukizi Rising Stars kila la kheri katika mashindano ya Afcon kwa chipukizi wakianza kampeini dhidi ya Morocco Mei 1.

Akizungumza kutoka Sweeden kupitia kanda ya video Mambo ameshukuru Rising Stars kupata nafasi hiyo ya kuakilisha taifa mjini Cairo akitaka wawe na ujasiri wasiogope timu yoyote.

“Kwanza Nishukuru Vijana wa Rising Stars pamoja na kocha Salim Babu,Hii ni fursa ya stars kuonyesha makali yao kwani mechi hizi ni kama mechi zingine,msiogope yeyote kwani tuna uwezo wa kushinda mtu yeyote kombe hili.”

Kulingana na Mambo ambaye kwa sasa amechukua mafunzo ya ukufunzi nchini Sweeden ni kwamba licha ya kundi hilo kuwa ngumu Rising stars hawafai kuonekana mnyonge hata kidogo kwa sababu wako kumi 11 uwnajani kama wenzao

“Msiogope yeyote kwani mmejitayarisha vya kutosha na ni muda wa kuenjoy na kushowcase vipaji vyenu kwa dunia. ” -Mambo.

Rising Stars wako kundi B pamoja na Morocco,Tunisia na Nigeria.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending