News
Mambo Atakia Kheri Rising Stars Misri Afcon u20

Kiungo wa zamani timu ya taifa ya soka Harambee Stars Robert Mambo ametakia vijana wa timu chipukizi Rising Stars kila la kheri katika mashindano ya Afcon kwa chipukizi wakianza kampeini dhidi ya Morocco Mei 1.
Akizungumza kutoka Sweeden kupitia kanda ya video Mambo ameshukuru Rising Stars kupata nafasi hiyo ya kuakilisha taifa mjini Cairo akitaka wawe na ujasiri wasiogope timu yoyote.
“Kwanza Nishukuru Vijana wa Rising Stars pamoja na kocha Salim Babu,Hii ni fursa ya stars kuonyesha makali yao kwani mechi hizi ni kama mechi zingine,msiogope yeyote kwani tuna uwezo wa kushinda mtu yeyote kombe hili.”
Kulingana na Mambo ambaye kwa sasa amechukua mafunzo ya ukufunzi nchini Sweeden ni kwamba licha ya kundi hilo kuwa ngumu Rising stars hawafai kuonekana mnyonge hata kidogo kwa sababu wako kumi 11 uwnajani kama wenzao
“Msiogope yeyote kwani mmejitayarisha vya kutosha na ni muda wa kuenjoy na kushowcase vipaji vyenu kwa dunia. ” -Mambo.
Rising Stars wako kundi B pamoja na Morocco,Tunisia na Nigeria.
News
Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.
Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.
Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.
Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.
“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.
Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.
Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.
“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.
Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.
Taarifa ya Janet Mumbi