Connect with us

News

Mahamoud Ali Ashinda Uchaguzi wa AUC

Published

on

Photo Courtesy

Mgombea wa wadhifa ya uwenyekiti wa Tume ya umoja wa Afrika AUC, Mahmoud Ali Youssouf kutoka Djibouti, sasa ndiye Mwenyekiti mpya wa Tume hiyo baada ya kushinda kwa kura 33 katika awamu ya 7.

Hii ni baada ya Raila Odinga kutoka Kenya kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho baada ya kushindwa na Mahmoud katika awamu ya tano na sita katika kinyang’anyiro hicho.

Mahmoud, ambaye katika awamu ya saba amepata kura 33, ambayo ni thuluthi mbili ya kura zote zilizopigwa katika ukumbi wa Nelson Mandela jijini Addis Ababa nchini Ethiopia, amepewa majukumu yake rasmi.

Wachanganuzi wa maswala ya kisiasa wameipongeza serikali ya Kenya kwa kuonyesha juhudi za kuyashawishi mataifa ya Afrika kumuunga mkono Odinga, japo matokeo hayakuridhisha.

Hata hivyo wanaogombea nafasi hiyo ilikuwa ni pamoja na Raila Odinga wa Kenya, Mahmoud Ali Youssouf wa Djibouti na Richard Randriamandrato wa Madagascar, huku mataifa ya Sudan, Burkina Faso, Mali, Gabon, Niger na Guinea yakifungiwa nje ya uchaguzi huo kutokana na vita katika mataifa hayo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wavuvi wawili wafa maji Watamu,Kilifi

Published

on

By

Jamii ya wavuvi katika eneo la Watamu eneo bunge la Kilifi Kaskazini inaiomba serikali ya kaunti ya Kilifi na ile ya kitaifa kununua boti za uokozi ili kusaidia kuokoa maisha wakati kunapotokea dharura baharini.

Hii ni baada ya wavuvi wawili kupotoea katika bahari hindi eneo la Watamu walipokuwa wakiendeleza shughuli zao za uvuvi siku ya Alhamisi 24, Julai 2025.

Kufikia sasa wawili hao hawajapatikana licha ya juhudi za wadau mbalimbali ikiwemo jeshi la wanamaji kuwatafuta.

Kiongozi wa vijana eneo la Watamu Bakari Shaban, alisema kuwa juhudi za kuwatafuta wavuvi hao ambao ni mandugu wanaotambulika kama Athman Lali na Huzefa Lali zinaendelea.

Shaban alisistiza haja ya serikali kuangazia suala la ununuzi wa mashua za kisasa za uokozi ili kupunguza visa vya wavuvi kuangamia baharini wakati wanapoelekea kuvua.

“Mpaka sasa juhudi zote zimefanyika lakini ndugu zetu hatujajua wako sehemu gani, serikali itusaidie mji wetu wa Watamu ni mji wa utalii, tunaomba tupate boti za kuokoa maisha baharini, popote alipo waziri Ali Joho angalau tupate boti za uokozi kama mbili hapa Watamu ni kitovu cha utalii kunamahoteli mengi, watalii wote wanaokuja Watamu mpaka leo hakuna boti za uokozi”, alisema Shaban.

Kwa upande wao wazazi wa wavuvi waliopotea baharini Lali Athman Lali na Dhurai Mohamed Ali waliiomba serikali kuweka juhudi zaidi za kuwasaidia kuwapata wana wao kwani ndio tegemeo kubwa kwa familia yao.

“Uko usaidizi unatumika, kuna vijana wanaojitolea kwa maboti wanaenda ile sehemu ambayo wavuvi wanavua, wanajaribu kuzunguka lakini toka siku hiyo hawajapata chochote: Katika Maisha yangu mimi nawategemea hawa watoto kunisomeshea hawa watoto wangu ambao ni wadogo zao mashule, kwa chakula kwa hivyo naomba serikali inisaidie kwa sababu ndio tegemeo langu hao watoto”.walisema wazazi.

Kisa hiki kinajiri miezi kadhaa baada ya mvuvi mmoja kutoka eneo la Mnarani mjini Kilifi kufariki baharini baada ya kugongwa kichwani kwa pondo na wavuvi wenzake kulipotokea mzozo kuhusu pato la samaki.

Kufikia sasa mwili wa mvuvi huyo haujapatikana

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Seneta Miraj apiga jeki mpango wa vitambulisho maalum Mombasa

Published

on

By

Seneta mteule katika kaunti ya Mombasa Miraj Abdillahi ameunga mkono mpango wa gavana wa kaunti hiyo Abdulswamad Shariff Nassir wa kuzindua vitambulisho maalumu kwa wenyeji wa kaunti ya Mombasa, ili wenyeji waweze kupata huduma mbalimbali kwa gharama nafuu na kwa urahisi.

Abdillahi ambaye alikuwa akizungumza katika eneo la Shika Adadu eneo  bunge la Likoni, kwenye hafla ya ugavi wa chakula, alisema hilo litawapunguzia wenyeji mahangaiko ambayo wamekuwa wakiyapitia kutokana na gharama za juu za matibabu katika kaunti ya Mombasa.

Kulingana na Miraj Abdillahi, wenyeji wamekuwa wakihangaika kutokana na gharama ya juu ya matibabu, chanzo kikuu kikiwa ni wawakilishi wa wadi wa kaunti ya Mombasa.

“Tumekuwa tukilia ya kwamba bili za hospitali ziko juu, si fitina na si siasa ikiwa mnataka bei ya huduma ya Coast General kushuka chini ongeeni na wawakilishi wa wadi wenu’’, Alisema Abdillahi.

Wakati huo huo, Abdillahi alitoa wito kwa wawakilishi wa wadi kutathmini sheria ambazo walibuni ili kupatikane mwafaka.

Haya yanajiri huku mvutano ukiendelea kushuhudiwa kati ya bunge la kaunti hiyo na serikali ya kaunti ya Mombasa kuhusiana na suala hilo.

Taarifa ya Janet Mumbi.

 

Continue Reading

Trending