Connect with us

News

Mahakama ya Mombasa Kusikiliza Kesi ya Mauaji ya Afisa wa IEBC

Published

on

Mahakama kuu ya Mombasa imeanza kuskiliza kesi ya mauaji ya aliyekuwa Kaimu Meneja wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC katika kaunti ya Kilifi Aisha Akinyi Abubakar.

Washtakiwa katika kesi hiyo, Joseph Sunday Otieno maarufu Brian Shikuku na Brian Templer Oyare wanakabiliwa na tuhuma za mauaji ya afisa huyo nyumbani kwake katika mtaa wa Utange eneo bunge la Kisauni katika kaunti ya Mombasa mnamo mwezi Januari tarehe 5 mwaka huu.

Wawili hao pia walishtakiwa kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi Mwanawe Marehemu na kutoweka na vifaa vya kieletroniki ikiwemo simu na vifaa vya IEBC, nyumbani kwao wakati wa tukio hilo.

Jaji Wendy Micheni ameanza kusikiliza kesi hiyo baada ya vipimo vya kiafya kutoka kwa madaktari kubaini kwamba washukiwa hao wawili wana akili timamu, hii ni baada ya Mahakama hapo awali kuagiza washukiwa hao wafanyiwe vipimo vya afya akili.

Oyare na Otieno wataendelea kufuatilia vikao vya kesi hiyo wakiwa rumande baada ya Mahakama kuwanyima dhamana kutokana na mashtaka yanayowakabili.

Kesi hiyo itaendelea kesho katika Mahakama hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending