Connect with us

National News

Mahakama Kuu Yamtupa Nje Gavana Mwangaza

Published

on

MAHAKAMANI – Gavana wa Meru Kawira Mwangaza amepata pigo baada ya Mahakama kuu kuidhinisha uamuzi wa bunge la Seneti la kumtimua Mamlakani.

Uamuzi huo imejiri baada ya bunge la Seneti kupiga kura kwa kauli moja na kuidhinisha malalamishi yaliowasilishwa na bunge la kaunti ya Meru dhidi ya kiongozi hiyo.

Malalamishi hayo dhidi ya Gavana Mwangaza ni pamoja na ukiukaji wa katiba, utumizi mbaya wa ofisi ya umma, ubadhirifu wa fedha miongoni mwa mashtaka mengine.

Akitoa uamuzi huo, Jaji wa Mahakama kuu Bahati Mwamuye, amesema Mahakama imeona kwamba ombi lililowasilishwa na Gavana Mwangaza la kupinga uamuzi wa bunge la Seneti halina uzito wowote na Mahakama ikatupilia mbali ombi hilo la Mwangaza.

“Mahakama hii imeona kwamba ombi lililowasilishwa na Gavana Mwangaza halina uhalali na kutulipiwa mbali. Notisi ya Gazeti la serikali iliyochapishwa tarehe 21 Agosti 2024 ya kumwondoa afisini imethibitishwa”, Jaji Mwamuye.

Mahakama imeamua kwamba bunge la Seneti halikukiuka maagizo yoyote ya Mahakama licha ya Gavana Mwangaza kulalamika kwamba bunge hilo liliegemea upande mmoja na kwamba Mahakama haikupata uthibitisho wowote juu ya madai hao.

Mahakama hata hivyo haikupata ushahidi wowote kwamba alinyimwa nafasi ya kuzungumza na ilibainisha kwamba timu yake ya mawakili haikuleta pingamizi lolote kuhusu muda uliotengwa kwa ajili ya utetezi wake.

Naibu Gavana wa kaunti hiyo ya Meru Isaac Mutuma M’Ethingia huenda akaapishwa rasmi na kuchukua nafasi ya Gavana katika kaunti hiyo ili kuhakikisha shughuli mbalimbali za kaunti zinaendelea vyema, iwapo Mwangaza hatakata rufaa kuhusu uamuzi huo wa Mahakama kuu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending