Connect with us

Sports

Madereva Wa KCB Kukabana Koo Rwanda Mountain Gorilla Rally

Published

on

Madereva zaidi ya 35 kuzindua uhasama katika makala ya mwaka huu ya Rwanda Mountain Gorilla Rally ikiwa ni raundi ya taji la Bara Afrika Julai 4 hadi Julai 6 mjini Kigali Rwanda.

Dereva wa Kenya Karan Patel amesema kwamba anatarajia upinzani mkubwa kutoka kwa Yasin Nasser raia wa Uganda ambaye amejinyakulia pointi 63 na ndiye anaongoza chati mashindano ya magari Barani Afrika,African Rally Championship.

Madereva wengine ambao wako kwenye kinyanganyiro cha kusaka taji hilo ni pamoja na Nikhil Sachania na Carl Flash Tundo ambao wote wanashika nafasi ya pili na alama 50.

Tineja Jeremiah Wahome ameketi nafasi ya nne na pointi 42 akifuatwa na Samman Vohra naye Karan Patel akiketi nafasi ya sita na pointi 35.

Madereva wengine watakaoshiriki ni Michael Muluka wa Uganda na Queen Kalimpinya wa Rwanda.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Rais Ruto Awapa Morale Kikosi Cha Stars Kambini

Published

on

By

Rais William Samoei Ruto mapema Leo ametembelea kikosi Cha timu ya Taifa Mpira wa Soka Harambee Stars Ugani Kasarani wanapofanyia mazoezi kwa Kombe la Chan 2025 mwezi ujao.
Hii ikiwa ni njia moja wapo ya kuwapa mortisha vijana wa nyumbani akiahidi Stars nchi nzima iko nyuma Yao.

Ruto amewatakia heri Stars na kuambia vijana wa nyumbani watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka kwake wanapo peperusha bendera ya taifa hili kwenye kipute cha CHAN mwezi ujao.

“Nataka tushinde kombe hili katika nchi yetu,kila Mkenya yuko nyuma yenu kuwapiga jeki ili mpate matokeo chanya mimi na serikali yangu tunahidi kuwapa sapoti yote kwa kombe hili.”

Rais aliandamana na Waziri wa Michezo Salim Mvurya pamoja na waziri wa Ulinzi Soipan Tuya.

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeini Agosti 3 dhidi ya DR. Congo ugani Kasarani ambapo watapiga mechi zao zote.

Continue Reading

Sports

Kasarani Na Nyayo:Uwezo Wa Kubeba Mashabiki Yapungua

Published

on

By

CHAN Siku 17 zimesalia kipute hicho kungoa nanga nchi za Kenya,Uganda na Tanzania.

Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo imetumia Kima Cha zaidi ya Shilingi Bilioni 6.7 kufanyia Ukarabati uwanja wa Kasarani na Shilingi nyingine Bilioni 1.1 Uga wa Nyayo.

Uwanja wa Kasarani Ulifungwa mwaka 2023 Kwa shughuli hiyo ya ukarabati huku uga wa Nyayo ukifungwa mwaka mmoja badaye 2024 kwa Maandalizi ya kipute cha CHAN kinachotarajiwa kung’oa nanga chini ya siku 17 zijazo.
Viwanja hivyo sasa vinauwezo wa kubeba mashabiki 55,000 na 22,000 mtawalia.
Ikumbukwe kabila ya ukarabati wa uwanja wa Kasarani ulikuwa na uwezo wa kuwabeba takriban mashabiki 60,000 huku uwanja wa Nyayo ukibeba mashabiki 30,000.
Continue Reading

Trending