Connect with us

News

LSK yamtaka Inspakta Kanja kuweka wazi kifo cha Ojwang’

Published

on

Chama cha mawakili nchini LSK kinamtaka Inspakta jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja kuhakikisha kuna uwazi kufuatia kifo tatanishi cha mwanablogu Albert Ojwang’.

Akihutubia Wanahabari siku ya Jumatatu, rais wa LSK Faith Odhiambo alimwagiza Kanja kutangaza majina ya maafisa ambao wanazuiliwa wakiwemo wale waliomsafirisha Ojwang’ kutoka kaunti ya Homabay hadi jijini Nairobi.

Kanja alitangaza kuzuiliwa kwa maafisa polisi waliokuwa zamu katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi wakati Ojwang’ alipowasilishwa kituoni ambapo baadaye alipatikana akiwa na majeraha mabaya ndani ya seli.

Odhiambo aliongeza kuwa taarifa iliyotolewa na Inspakta Jenerali Douglas Kanja kuhusu kifo cha mwanablogu huyo haitosheleza kufafanua yaliyojiri.

“Kwa nini hajataja majini ya maafisa waliozuiliwa? Mbona anaficha? Wacha wakenya wafahamu. Tunataka kujua maafisa waliomchukuwa Ojwang’ je wao ni miongoni mwa wanaozuiliwa?”, alisema Odhiambo.

Rais huyo wa LSK pia alilaumu jinsi maafisa wa usalama walivyomshikilia Ojwang’ hadi akakutana na mauti yake

“Jinsi walivyomhudumia Albert Ojwang’ ni ukiukaji wa haki zake pamoja na wananchi wakenya. Hiki hakiwezi kuchukuliwa kama kisa cha kawaida kwa sababu kinaashiria namna mamlaka inavyohudumu ndani ya huduma ya maafisa wa polisi”, aliongeza rais wa LSK.

Wakati huo huo waanadamanaji pamoja na wanaharakati walikusanyika nje ya makafani ya City jijini Nairobi wakishinikiza hatua za haraka kuchukuliwa kuhusiana na kisa hicho.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending