Connect with us

Business

KPA yatoa ilani ya siku 14 kwa kampuni za meli

Published

on

Mamlaka ya bandari nchini KPA imeanzisha zoezi la kusafisha maeneo ya kuhifadhi mizigo katika bandari ya Mombasa katika juhudi za kuboresha utoaji wa huduma na kuhakikisha usalama na ufanisi wa shughuli za bandari,.

Taarifa rasmi ya KPA ilisema kuwa, baada ya ukaguzi wa kina baadhi ya makasha na mizigo bado yanasalia bandarini licha ya kuamuliwa kuwa yamekataliwa kwa mujibu wa sheria na hivyo yanapaswa kuondolewa au kuharibiwa.

KPA sasa inazipa kampuni za meli muda wa siku 14 kuhakikisha zinashughulikia uondoaji au uharibifu wa mizigo hiyo.

Mamlaka hiyo ilisisitiza kuwa endapo muda huo utapita bila hatua kuchukuliwa, bandari italazimika kuharibu au kuondoa mizigo hiyo kwa gharama ya kampuni husika, bila kuwahusisha tena wamiliki wa mizigo hiyo.

Hatua hii inalenga kuongeza nafasi bandarini na kuhakikisha huduma bora kwa wateja wanaotegemea bandari ya Mombasa kusafirisha na kupokea bidhaa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Mradi wa kiuchumi wa Dongo Kundu wavutia wawekezaji zaidi

Published

on

By

Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaendelea kuonyesha nia ya kuekeza katika mradi wa kiuchumi wa dongo kundu kaunti ya Mombasa.

Mradi huo unaotarajiwa kuongeza uzalishaji katika viwanda na thamani ya bidhaa ndani ya nchi na nje, unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Kampuni ya nishati kutoka China, Ruike Energy Group Limited, ni mwekezaji wa hivi karibuni kuonyesha nia ya kupata nafasi ndani ya eneo hilo la kiuchumi la Dongo Kundu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta.

Kulingana na halmashauri ya bandari nchini KPA hatua hiyo italeta faida Zaidi ikiwemo kubuni nafasi za ajira, ikuaji wa uchumi, upatikanaji wa vifaa vya baharini, na urahisi wa kufikia masoko ya kanda na ya kimataifa.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

KETRACO kuimarisha usalama wa chakula nchini

Published

on

By

Shirika la usambazaji umeme nchini, KETRACO, limethibitisha dhamira yake ya kuimarisha usalama wa chakula, ukuaji wa kijani, na ushirikiano wa kieneo kupitia uekezaji mkubwa katika miundombinu ya umeme.

Katika maonesho ya Kimataifa ya kilimo ASK yanayoendelea kaunti ya Mombasa, KETRACO imeonyesha jinsi miundombinu yake ya umeme inavyowezesha kilimo cha kisasa na uzalishaji wa viwandani.

Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi mkuu, mhandisi Kipkemoi Kibias, KETRACO imekamilisha miradi 43 ya njia za kusafirisha umeme, huku mingine 29 ikitarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2028.

Kibias, alisema shirika hilo tayari limejenga zaidi ya kilomita elfu sita za njia za umeme wa msongo mkubwa, likiwa pia na vituo 46 vya kusambaza umeme na upanuzi wa mitambo 33.

Katika eneo la Pwani, Kibias alisema upanuzi wa mpango wa Green Energy Backbone umewezesha usambazaji wa kawi safi kwa asilimia 93, jambo lililopunguza utegemezi wa mafuta na kuchochea maendeleo ya biashara za kilimo, utalii na uchumi wa baharini.

Kibias alisema KETRACO inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuunganisha Kenya na nchi jirani kupitia njia za kimataifa kama zile za Ethiopia, Tanzania na Uganda hatua zitakazowezesha biashara ya umeme Afrika Mashariki.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending