Connect with us

News

Kongamano la kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia Taita Taveta

Published

on

Idara ya usalama kaunti ya Taita taveta imeandaa kongamano maalum ili kujadili namna ya kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia na kingono kaunti hiyo.

Kongamano hilo limefanyika katika eneo la Werugha, eneo bunge la Wundanyi kaunti ya Taita Taveta na limejumuisha maafisa wakuu wa serikali ya kaunti hiyo, viongozi wa kijamii pamoja na wananchi.

Kamishna wa kaunti ya Taita Taveta Josephine Onunga alibainisha kuwa kuna ongezeko la visa 186 ndani ya miaka miwili, eneo bunge la Taveta likirekodi visa 64 huku Wundanyi ikirekodi 38 hivyo kuwataka wakaazi kushirikiana na idara mbalimbali za usalama ili kukomesha visa hivyo.

“Tunapendekeza ushirikiano mkubwa zaidi na zaidi kuanzia mashinani kila boma tulindane, tujuliane hali, hakikisha unamlinda mwenzako”, alisema Onunga.

Kwa upande wao Wanaharakati wa kupambana na dhuluma za kijinsia wakiongozwa na Mary Mgola walieleza hofu yao kutokana na ongezeko la visa hivyo hasa maeneo ya mashinani.

Walisema ukosefu wa mashahidi wa kutosha wakati kesi hizo zinapowasilishwa Mahakamani, ikitajwa kama changamoto kuu wakati wa kusuluhisha kesi hizo.

Mgola aliitaka Mahakama kuhakikisha wanatoa ulinzi wa kutosha kwa mashahidi wa kesi za dhuluma za kijinsia na kingono.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending