Connect with us

Sports

Kocha Wa Stars Mccarthy Ataja Kikosi Cha Mwisho Kombe La CHAN

Published

on

Mkufunzi wa timu ya soka Harambee Stars Benni Mccarthy amekitaja kikosi chake cha mwisho chenye wachezaji 25 tayari kwa kombe la Chan mwezi ujao,vijana wa nyumbani wakifungua dimba dhidi ya DR.Congo Agosti 3 ugani Kasarani.

Miongoni mwa nyota waliojumuishwa kikosini ni pamoja na kipa mzoefu wa kilabu ya Bandari FC Faruk Shikhalo,beki wa Police Aboud Omar ambaye atakua nahodha wa kikosi hicho pamoja na viungo Austine Odhiambo,Marvin Nabwire na mshambulizi Masoud Juma ataongoza safu ya mashambulizi pamoja na Ryan Ogam wa kilabu ya Tusker Fc.

Magolikipa;

Faruk Shikhalo, Byrne Omondi, Sebastian Wekesa

Mabeki;
Siraj Mohammed, Manzur Suleiman, Pamba Swaleh, Abud Omar, Alphonce Omija, Sylvester Owino, Mike Kibwage, Daniel Sakari, Lewis Bandi, Kevin Okumu

Viungo;
Brian Musa, Alpha Onyango, Austin Odhiambo, Ben Stanley, Marvin Nabwire

Washambulizi;
Mohammed Bajaber, Boniface Muchiri, David Sakwa, Ryan Ogam, Masoud Juma, Austin Odongo, Felix Oluoch

Stars wako kundi A pamoja na Angola,DR.Congo,Morocco na Zambia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Msururu Wa Raga Driftwood 7s Umengoa Nanga Mombasa

Published

on

By

Mashindano ya kitaifa ya misururu ya Raga nchini mwaka 2025 yameongoa nanga mjini Mombasa, Msururu huo wa kwanza wa Driftwood 7s inafanyika katika uwanja wa Mombasa Sports Club.

Jumla ya timu 26 zinashiriki katika makundi ya wavulana na wasichana wa chini ya umri wa miaka 18 na 15, na kundi la pamoja kwa walio chini ya miaka 13, yakionyesha kizazi kipya cha vipaji vya raga nchini Kenya.

Katika mashindano ya Divisheni ya Kwanza, mabingwa watetezi Kenya Harlequins wako Kundi A dhidi ya MMUST, KU Blak Blad, na Mwamba RFC,

Kundi B linajumuisha Kabras Sugar RFC,Catholic Monks, Nakuru RFC, na Impala RFC, kundi C linajumuisha KCB RFC, Nondescripts RFC, Daystar Falcons, na wenyeji MSC Rugby huku Kundi D litakuwa na ushindani mkali kati ya Menengai Oilers, Strathmore Leos, Stallions Rugby, na Kabarak University.

Kwa upande wa Division Two, timu 36 zinashiriki katika mashindano hayo, ambapo vigezo maalum vilitumika kugawa nafasi kwa vilabu wanachama wa KRU, timu kutoka ukanda wa pwani, zile zilizofanya vizuri awali, na zile zenye historia nzuri katika mashindano.

Makundi ya Division Two ni pamoja na AP Warriors, Kilifi Titans, Likoni, na Mean Machine ambao watacheza katika Kundi A; Embu RFC, Kaya Rugby, North Coast Stormers, na MKU Thika katika Kundi B; Homeboyz RFC, Jackals, NYS Eagles, na Makueni RFC katika Kundi C; Kisumu RFC, KCNP, NYS Spades, na Sigalagala NP katika Kundi D; huku South Coast Pirates, Vihiga Granites, Zetech Oaks, na Northern Suburbs wakicheza katika Kundi E.

Mechi ya fainali ya mashindano hayo itachezwa siku ya Jumapili mwaka huu.

Continue Reading

Sports

Kocha Wa Bafana Bafana Ataja Kikosi Cha Mwisho Cha CHAN

Published

on

By

AFRIKA KUSINI (SOUTH AFRICA)

Wanajiita Bafana Bafana kwa jina la Utani.
Afrika Kusini inaorodheshwa ya 56 msimamo wa kila mwezi wa shirikisho la soka ulimwenguni FIFA
Taifa hilo halijawahi kushinda taji la CHAN licha ya kushiriki mara tatu miaka ya  (2011, 2014, 2025)

Kocha mkuu wa taifa hilo anaitwa Hugo Broos Hata hivyo katika majukumu ya CHAN amepewa kocha Molefi Ntseki ambaye ni mchezaji wa zamani wa taifa hilo na pia amewahi kuvinoa vikosi vya wachezaji wachanga timu ya taifa pamoja na vilabu vya Kaizer Chiefs na Bloemfontein.
Kocha huyo ametaja wachezaji 14 ambao hawana vilabu katika kikosi alichokitaja cha wachezaji 25
Badhi ya wachezaji nyota ni pamoja na Neo Maema anayepiga na Mamelodi Sundowns.
Bafana Bafana wako kundi C pamoja na Algeria,Guinea,Niger na Uganda.
Continue Reading

Trending