Connect with us

Sports

Kocha wa Stars Benni Mccarthy Ana Imani Kupata Ushindi dhidi ya Madagascar Robo Fainali CHAN Kasarani

Published

on

Kocha mkuu wa Harambee Stars, Benni McCarthy, ameonyesha imani kubwa huku kikosi chake kikijiandaa kwa pambano la kihistoria la robo fainali dhidi ya Madagascar litakalochezwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani, Ijumaa, Agosti 22 saa 11 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari kabla ya mechi akiwa ameandamana na nahodha msaidizi Daniel Sakari, McCarthy amesema safari ya Stars katika hatua ya makundi imewaimarisha kwa hatua ya muondoano.

Kenya iliongoza katika kundi gumu lililojumuisha DR Congo, Angola, Morocco na Zambia na kufanikisha tiketi ya kufika robo fainali.
“Baada ya mtihani tulioupitia hatua ya makundi, nafikiri hakuna timu ambayo tunaogopa tena. Fursa zetu zilikuwa finyu, lakini tulijithibitisha kwamba tuna uwezo wa kuvuka vikwazo hivyo. Yeyote atakayekuja mbele yetu atakuwa changamoto nzuri, lakini mtazamo wetu ni sisi wenyewe na kusonga hatua inayofuata,” alisema McCarthy.

Mtaalamu huyo kutoka Afrika Kusini alibainisha maandalizi yake yanahusisha zaidi ya mbinu, akisisitiza uimara wa kisaikolojia.

“Nafanya kazi ya kujenga utulivu wa kiakili ndani ya wachezaji wangu. Matumaini yako juu, lakini tulifanya uchambuzi wetu wa wapinzani watarajiwa. Madagascar watakuwa kizuizi kingine, na haijalishi tulichokipata kabla, kimesahaulika. Tunapaswa kujiandaa kadiri tuwezavyo,” alisisitiza McCarthy.

McCarthy alithibitisha kuwa hakuna majeraha makubwa kuelekea robo fainali. Mchezaji pekee atakayekosa ni Chrispine Erambo, aliyesimamishwa baada ya kadi nyekundu wakati wa ushindi wa Stars wa 1-0 dhidi ya Morocco.

Akitambua ubora wa kipa Byrne Omondi aliyeibuka shujaa wa mechi, McCarthy aliwataka wachezaji wake kuongeza makali ya safu ya ushambuliaji.

Ushindi dhidi ya Madagascar utaipeleka Kenya kwenye nusu fainali dhidi ya mshindi kati ya Algeria na Sudan watakaovaana Jumamosi, Agosti 23, kule Zanzibar.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Published

on

By

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.

WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.

Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.

Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:

  • Urusi

  • Sri Lanka

  • Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota

  • Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)

Continue Reading

Sports

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Published

on

By

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.

Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.

Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.

Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.

Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.

“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”

Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.

Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.

Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.

Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.

Continue Reading

Trending