Connect with us

Sports

Kocha Wa Starlets Odemba ajiuzulu

Published

on

Mkufunzi wa timu ya taifa soka akina dada Harambee Starlets Beldine Odemba ametangaza kujizulu wadhifa wake kama kocha mkuu wa kikosi hicho baada ya kichapo cha magoli 5-1 na Morocco mechi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kilichomfanya kuondoka katika kambi ya timu hiyo ni kukosa ungwaji mkono katika kazi yake ya kunoa starlets akiondoka siku chache tuu kabla ya kungoa nanga kwa taji Cecafa nchini Tanzania Juni 12.

Mkufunzi huyo ambaye ameshinda ligi ya akina dada na kilabu ya Kenya Bullets amedokeza kwamba ni swala ambalo ameliwazia kwa muda na kwa sasa anaelekeza nguvu zote kwa kikosi hicho taji la Cecafa baina ya vilabu.

Ripoti zinaarifu kwamba kocha wa Kibera Soccer Women David Vijago atatangazwa kocha mpya wa Starlets akisaidiana na Alex Alumira ambaye amewahi kuwa kocha wa timu hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending