Connect with us

News

KNUT Yaitataka TSC kutekeleza CBA wa mwaka, 2025/2029

Published

on

Naibu Katibu mkuu wa Chama cha kutetea maslahi ya walimu nchini KNUT Hesbon Otieno aliitaka Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuyapa kipau mbele mazungumzo ya makataba wa makubaliano wa malipo nchini CBA wa mwaka wa 2025/2029.

Hesbon alisema suala hilo linafaa kuchukuliwa kama la dharura, akimtaka Kaimu Afisa mkuu mtendaji wa Tume hiyo Evaleen Mitei kuhakikisha suala hilo linatekelezwa kwani CBA ya sasa haina manufaa yoyote ya kifedha kwa walimu.

Akizungumza katika kaunti ya Kericho, Hesbon alisema KNUT inadai ongezeko la asilimia 60 ya mishahara na ongezeko la asilimia 30 kama marupurupu kwa walimu wote nchini, akisisitiza haja ya ongezeko hilo la mshahara kutekelezwa.

“Tulifanya mazungumzo na TSC kwa muda mrefu na kuafikia nyongeza ya asilimia 60 ya mishahara kwani ile CBA ya sasa inaisha Juni na haina manufaa kwa walimu, ndio maana tunaiambia TSC itekeleza makubaliano ya CBA”, alisema Hesbon.

Itakumbukwa kwamba viongozi wa KNUT na TSC waliwahi kuwa katika mazungumzo ya zaidi ya mwaka mmoja na iwapo yatatekelezwa basi changamoto zinazowakumba walimu zitapungua.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending