Connect with us

Sports

Klabu ya KCB yatwaa ubingwa wa Raga ya Driftwood 7s mjini Mombasa

Published

on

Klabu ya KCB ndiyo mabingwa wa michuano ya Raga ya wachezaji saba kila upande ya Driftwood 7s iliyofanyika mjini Mombasa.

Hii ni baada ya kuibuka na ushindi wa alama 15–14 dhidi ya klabu ya Strathmore Leos katika fainali ya kusisimua iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mombasa Sports Club.

KCB, maarufu kama Mabenki, walianza mchezo kwa kasi na kutawala kipindi cha kwanza. Hata hivyo, Strathmore walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na walikuwa karibu kusawazisha, lakini walikosa kwa pointi moja pekee.

Katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu, Kabras RFC waliibuka na ushindi wa alama 21–10 dhidi ya Nakuru RFC, na hivyo kupanda kutoka nafasi ya nne waliyoshikilia mwaka 2024.

Wakati huo huo, katika Divisheni ya Pili, Zetech Oaks waliibuka kidedea kwa kuichapa NYS Spades kwa alama 10–0, na kutwaa ubingwa bila kuruhusu bao lolote.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Morocco ‘Atlas Lions’ Yawasili Nairobi kwa Mashindano ya CHAN

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Morocco, maarufu kama The Atlas Lions, imewasili jijini Nairobi tayari kwa mashindano ya CHAN yatakayofanyika mwezi ujao katika viwanja vya Nyayo na Kasarani.

Kikosi hicho chenye wachezaji 25 pamoja na benchi la kiufundi kilipokelewa vyema katika uwanja wa ndege kabla ya kuelekea hotelini, tayari kwa maandalizi ya mashindano hayo.

Morocco iko katika Kundi A pamoja na wenyeji Kenya, Angola, Zambia, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo).

Continue Reading

Sports

Msururu Wa Raga Driftwood 7s Umengoa Nanga Mombasa

Published

on

By

Mashindano ya kitaifa ya misururu ya Raga nchini mwaka 2025 yameongoa nanga mjini Mombasa, Msururu huo wa kwanza wa Driftwood 7s inafanyika katika uwanja wa Mombasa Sports Club.

Jumla ya timu 26 zinashiriki katika makundi ya wavulana na wasichana wa chini ya umri wa miaka 18 na 15, na kundi la pamoja kwa walio chini ya miaka 13, yakionyesha kizazi kipya cha vipaji vya raga nchini Kenya.

Katika mashindano ya Divisheni ya Kwanza, mabingwa watetezi Kenya Harlequins wako Kundi A dhidi ya MMUST, KU Blak Blad, na Mwamba RFC,

Kundi B linajumuisha Kabras Sugar RFC,Catholic Monks, Nakuru RFC, na Impala RFC, kundi C linajumuisha KCB RFC, Nondescripts RFC, Daystar Falcons, na wenyeji MSC Rugby huku Kundi D litakuwa na ushindani mkali kati ya Menengai Oilers, Strathmore Leos, Stallions Rugby, na Kabarak University.

Kwa upande wa Division Two, timu 36 zinashiriki katika mashindano hayo, ambapo vigezo maalum vilitumika kugawa nafasi kwa vilabu wanachama wa KRU, timu kutoka ukanda wa pwani, zile zilizofanya vizuri awali, na zile zenye historia nzuri katika mashindano.

Makundi ya Division Two ni pamoja na AP Warriors, Kilifi Titans, Likoni, na Mean Machine ambao watacheza katika Kundi A; Embu RFC, Kaya Rugby, North Coast Stormers, na MKU Thika katika Kundi B; Homeboyz RFC, Jackals, NYS Eagles, na Makueni RFC katika Kundi C; Kisumu RFC, KCNP, NYS Spades, na Sigalagala NP katika Kundi D; huku South Coast Pirates, Vihiga Granites, Zetech Oaks, na Northern Suburbs wakicheza katika Kundi E.

Mechi ya fainali ya mashindano hayo itachezwa siku ya Jumapili mwaka huu.

Continue Reading

Trending