Connect with us

News

Kimotho: Deni lililosalia kwa waathiriwa wa bwawa la Mwache ni shilingi bilioni 2

Published

on

Serikali imesema itakamilisha malipo ya fidia kwa waathiriwa wote wa ujenzi wa mradi wa Bwawa la Mwache katika eneo la Kinango kaunti ya Kwale ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Katibu katika Idara ya unyunyizaji maji nchini Ephastus Kimotho amesema deni lililosalia kwa waathiriwa wa mradi huo ni shilingi bilioni 2 na tayari limeanza kulipwa.

Kimotho amesema hatua hiyo imeafikiwa baada ya Tume ya kitaifa ya ardhi NLC kupewa shilingi milioni 600 ambazo zitapewa waathiriwa kama fidia kuanzia wiki ijayo.

Akizungumza baada ya kutembelea mradi huo sawa na kuzindua kituo cha afya cha Mazeras kinachojengwa kama sehemu ya mradi huo, Kimotho amesema fedha zilizosalia zitaanza kutolewa kuanzia mwezi Julai ili kuafikia mipango iliyowekwa.

“Kufikia mwezi Julai mwaka huu tutakuwa tumeanza kusambaza mgao mwengine wa fedha zilizosalia ili kukamilisha fidia hizo kufikia mwezi Disemba mwaka huu”, alisema Kimotho.

Shughuli za ujenzi wa Bwawa la Mwache

Kwa upande wake Gavana wa Kwale Fatuma Achani amesema mradi huo uko na manufaa mengi kwa wakaazi wa kaunti ya Kwale ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya, shule, miongoni mwa manufaa mengine.

“Tumeona manufaa mengi kupitia mradi huu, umeleta vituo vya afya karibu na wananchi, ujenzi wa shule za Chekechea na miradi mingi muhimu ya umma, hivyo basi tunafaa kuunga mkono kikamilifu”, alisema Gavana Achani.

Mradi huo ambao ulikuwa umetengewa shilingi bilioni 4.6 kama fidia ya wakaazi waliopeyana ardhi zao kwa ujenzi wa mradi huo zimekuwa zilipiwa kwa njia ya awamu hali ambayo ilisababisha maandamano kutokana na kucheleweshwa kwa fidia hiyo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Sekta ya boda boda nchini kudhibitiwa na sheria kali

Published

on

By

Sekta ya boda boda nchini sasa itakuwa inadhibitiwa na sheria kali, ikiwemo usajili mpya unaoonyesha maeneo maalum ya vituo pamoja na sare za rangi tofauti kulingana na maeneo wanayohudumu.

Hatua hizi zinalenga kukabiliana na ongezeko la visa vya uhalifu na uteketezaji wa magari ya watu binafsi na wanaboda boda.

Kulingana na kamanda wa Polisi jijini Nairobi George Seda kila kituo pia kitahitajika kuwa na mwenyekiti ambaye atawajibika na kukamatwa, tukio likitokea eneo hilo na likihusisha wanaboda boda.

Kulingana na kaununi mpya wahudumu hao watapewa usajili mpya kando na ule wa nambari za NTSA unaoonyesha wanapofanya kazi, kuanzia kaunti, kaunti ndogo hadi kituo cha abiria.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

David Maraga amfokea mkurugenzi wa mashtaka ya umma

Published

on

By

Jaji mkuu mstaafu David Maraga amefokea ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kwa kuwashtaki kwa makosa ya ugaidi vijana waliokamatwa wakati wa maandamano.

Maraga alisema hatua hiyo inawadhulumu vijana hao ambao wamesalia korokoroni wakisubiri kesi yao kuamuliwa.

Maraga pia aliaka kesi hizo zitupiliwe mbali akisema hazina msingi, akidai hatua hiyo ni utumizi mbaya wa sheria kwa madai ya kukabiliana na magaidi, ilihali walioshtakiwa walikuwa wakishinikiza uongozi bora nchini.

Maraga pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za binadam walimtaka mkurugenzi wa mashtaka ya umma Renson Ingonga kuwajibika na kutupilia mbali kesi hizo na kuwaruhusu washukiwa kuendelea na maisha yao.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending