News
Kilabu Ya Barcelona Yakabwa Koo UEFA

Miamba wa Uhispania kilabu ya Barcelona kina kibarua kigumu mechi ya mkondo wa pili nchini Italia baada ya kutoka sare ya magoli 3-3 dhidi ya Intermilan mechi ya mkondo wa kwanza ugani Estadio Olympic St.luis Companys siku ya jumatano.
Mshambulizi wa Ufaransa Marcus Thuram alihitaji dakika moja pekee kuwaweka uongozini vijana wa kocha Simeone Inzaghi baada ya pasi murwa kutoka kwa beki Denzil Dumfries ambaye aliongeza la pili dakika 20 badaye na kufanya mambo kuwa magoli 2-0
Hata hivyo Barcelona walikua na jambo lao wakipiga comeback ya haraka haraka kupitia winga matata tineja Lamine Yamal kunako dakika ya 24 kabla ya Ferran Torres kuweka mambo sawa dakika ya 38.
Hata hivyo licha ya kuchukua uongozi tena kupitia goli lake Denzel Dumfries dakika ya 63 The Catalans walihitaji dakika moja kusawazisha kupitia goli la kujifunga la kipa Yan Sommer baada ya mkwaju kali ilitumwa kimyani na winga wa Brazil Raphinha kunako dakika ya 64.
Mshambulizi Lamine Yamal akiwa na umri wa miaka 17 alikua anashiriki mechi yake ya 100 tangu anze kuchezea vinara hao wa Laliga.
Mechi ya mkondo wa pili itapigwa siku ya jumanne ugani San siro ambapo yeyote ana uwezo wa kupiga hatua kwenye nusu fainali hiyo.
News
Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo.
Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.
Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.
Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.
Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.
Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.
Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.
“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.
Taarifa ya Hamis Kombe