Connect with us

News

Kilabu Ya Barcelona Yakabwa Koo UEFA

Published

on

Miamba wa Uhispania kilabu ya Barcelona kina kibarua kigumu mechi ya mkondo wa pili nchini Italia baada ya kutoka sare ya magoli 3-3 dhidi ya Intermilan mechi ya mkondo wa kwanza ugani Estadio Olympic St.luis Companys siku ya jumatano.

Mshambulizi wa Ufaransa Marcus Thuram alihitaji dakika moja pekee kuwaweka uongozini vijana wa kocha Simeone Inzaghi baada ya pasi murwa kutoka kwa beki Denzil Dumfries ambaye aliongeza la pili dakika 20 badaye na kufanya mambo kuwa magoli 2-0

Hata hivyo Barcelona walikua na jambo lao wakipiga comeback ya haraka haraka kupitia winga matata tineja Lamine Yamal kunako dakika ya 24 kabla ya Ferran Torres kuweka mambo sawa dakika ya 38.

Hata hivyo licha ya kuchukua uongozi tena kupitia goli lake Denzel Dumfries dakika ya 63 The Catalans walihitaji dakika moja kusawazisha kupitia goli la kujifunga la kipa Yan Sommer baada ya mkwaju kali ilitumwa kimyani na winga wa Brazil Raphinha kunako dakika ya 64.

Mshambulizi Lamine Yamal akiwa na umri wa miaka 17 alikua anashiriki mechi yake ya 100 tangu anze kuchezea vinara hao wa Laliga.

Mechi ya mkondo wa pili itapigwa siku ya jumanne ugani San siro ambapo yeyote ana uwezo wa kupiga hatua kwenye nusu fainali hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mudavadi: Mazungumzo yanaendelea kuhusu mzozo wa Kenya na Tanzania

Published

on

By

Mzozo kati ya Kenya na Tanzania umeanza kutokota kufuatia ilani iliyotolewa siku ya Jumanne Julia 29, na serikili ya Muungano wa Jumhuri ya Tanzania.

Serikali hiyo ya Tanzania kupitia Waziri wa Biashara na viwanda nchini humo Selemani Jefo ilitoa ilani ya kuwazuia wafanyibiashara wa kigeni kuendelea kufanya baadhi ya biashara katika taifa hilo.

Kutokana na hilo, Waziri wa masuala ya kigeni nchini Musalia Mudavadi alisema juhudi zimeanza za kuishawishi serikali ya Tanzania kuondoa vikwanzo hivyo na kwamba Rais William Ruto anafanya mazungumzo na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu suala hilo.

“Rais William Ruto ambaye ni Mwenyekiti wa Jumaiya ya Afrika Mashariki anafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na mwafaka utapatikana kwani pia suala la diplomasia ni mwafaka na hii tatizo tutatua kama serikali kupitia mazungumzo ya kidiplomasia”, alisema Mudavadi.

Kwa upande wake Waziri wa biashara na viwanda nchini Lei Kinyanjua alionya kwamba huenda serikali ya Kenya ikachukua hatua sawa na hiyo dhidi ya Tanzania iwapo taifa hilo la Afrika Mashariki halitaangazia upya vikwanzo hivyo.

Mzozo huo wa kidiplomasia umejiri siku moja tu baada ya Waziri wa biashara na viwanda nchini Tanzania Selemani Jafo kutangaza kwamba serikali ya Tanzania imepiga marufuku wafanyibiashara wa kigeni dhidi ya kufanya biashara ndogo ndogo nchini humu ili kuruhusu watanzania kujiimarisha kiuchumi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Ethekon: Sheria haijafafanua taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeweka wazi kwamba hakuna sheria inayofafanua misingi na taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi.

IEBC, ilieleza kwamba suala hilo ni kinyume cha Katiba na ubaguzi ikilinganisha hatua hiyo na uamuzi uliyotolewa na Mahakama kuu kuhusu kesi iliyowasilishwa Mahakamani na Taasisi ya Katiba dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria mkuu kwa kuambatana na sheria ya uchaguzi ya 2011.

Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon, IEBC ilisema kutokana na kwamba hakuna mfumo wa sheria wa kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi, wakenya wanaweza kutumia kipengele cha 104 cha Katiba na kuwarudisha nyumbani Wawakilishi wadi. 

Aidha alisema wakati bunge la kitaifa likifanya marekebisho ya sheria kuruhusu kurudishwa nyumbani Wawakilishi wadi, hakuna mwafaka wowote uliafikiwa wa kuruhusu wabunge kurudishwa nyumbani iwapo wamekosa kuwajibika. 

Hata hivyo Tume hiyo imeahidi kuwajibika kikamilifu katika suala hilo huku ikisema tayari imeliandikia barua bunge la kitaifa kuibuka na sheria ya kuwarudisha nyumbani wabunge wasiowajibika.

Haya yamejiri kufuatia malalamishi yaliowasilishwa na baadhi ya wakenya wanaotaka baadhi ya wabunge na maseneta kurudishwa nyumbani wa hivi karibuni akiwa Mwakilishi wa Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris akituhumiwa kuvunja sheria na kukiukaji wa Katiba lakini uamuzi wa Tume ya IEBC ni afuani kwake.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending