Connect with us

News

Kesi ya Wakili Joseph Munyithia na Farid Salim Yachukua Mkondo Mpya

Published

on

Kesi ya wizi wa ardhi inayomuhusisha Wakili Joseph Munyithia na mfanyabiashara Farid Salim Almaary imechukua mkondo mpya.

Hii ni baada ya mwanasheria huyo kuandikisha taarifa katika kituo cha polisi cha Makupa mjini Mombasa akijitenga na madai ya wizi wa kipande hicho cha ardhi kilichoko katika eneo la Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Katika taarifa yake kwa Polisi, Munyithia ameeleza kwamba alishughulikia ardhi hiyo ambayo alikabidhiwa hatimiliki na Gabriel Mutiso ambaye kwa sasa ni marehemu.

Aidha ameeleza kwamba mnamo Machi tarehe 4 mwaka 2024 alipeana cheti cha kukodisha shamba hilo pamoja na barua ya uhamisho hadi kwa kampuni ya J Katisya and Co Advocates.

Wakili huyo mkuu katika kampuni ya Munyithia, Mutugi na Umazi Advocates ameandikisha taarifa takriban wiki moja baada ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma nchini ODPP, kuagiza kukamatwa kwake pamoja na mfanyabiashara Farid.

Munyithia pamoja na mfanyabiashara huyo wanadaiwa kuiba na kuficha hati miliki ya ardhi hiyo kulingana na malalamishi yaliowasilishwa na wamiliki wa shamba hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

KNUT Yaitataka TSC kutekeleza CBA wa mwaka, 2025/2029

Published

on

By

Naibu Katibu mkuu wa Chama cha kutetea maslahi ya walimu nchini KNUT Hesbon Otieno aliitaka Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuyapa kipau mbele mazungumzo ya makataba wa makubaliano wa malipo nchini CBA wa mwaka wa 2025/2029.

Hesbon alisema suala hilo linafaa kuchukuliwa kama la dharura, akimtaka Kaimu Afisa mkuu mtendaji wa Tume hiyo Evaleen Mitei kuhakikisha suala hilo linatekelezwa kwani CBA ya sasa haina manufaa yoyote ya kifedha kwa walimu.

Akizungumza katika kaunti ya Kericho, Hesbon alisema KNUT inadai ongezeko la asilimia 60 ya mishahara na ongezeko la asilimia 30 kama marupurupu kwa walimu wote nchini, akisisitiza haja ya ongezeko hilo la mshahara kutekelezwa.

“Tulifanya mazungumzo na TSC kwa muda mrefu na kuafikia nyongeza ya asilimia 60 ya mishahara kwani ile CBA ya sasa inaisha Juni na haina manufaa kwa walimu, ndio maana tunaiambia TSC itekeleza makubaliano ya CBA”, alisema Hesbon.

Itakumbukwa kwamba viongozi wa KNUT na TSC waliwahi kuwa katika mazungumzo ya zaidi ya mwaka mmoja na iwapo yatatekelezwa basi changamoto zinazowakumba walimu zitapungua.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Kalonzo, Gachagua Wapinga Ujenzi wa Kinu cha Nuklia Kilifi

Published

on

Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, wamepaza sauti kupinga ujenzi wa kinu cha Nuklia katika eneo la Uyombo wadi ya Matsangoni Kaunti ya Kilifi.

Wakihutubu mjini Malindi Kaunti ya Kilifi viongozi hao akiwemo kinara wa DCP, aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua na mwenzake wa DAP, Eugene Wamalwa, waliongeza kwamba tayari wamewaagiza mawakili kuwasilisha kesi mahakamani kupinga mradi huo.

Waliyasema haya baada ya kuhudhuria misa ya Jumalipili katika katika Kanisa la JCC iliyoongozwa na Askofu Kakala mjini humo katika siku ya pili ya ziara yao ya ukanda wa Pwani.

Kalonzo alizidisha makombora yake Kwa serikali ya Rais William Ruto akiitaka iwajibikie maovu yake ya visa vya utekaji nyara na mauaji ya Vijana wa kizazi cha Gen-Z wakati wa Maandamano mwaka uliopita.

Kiongozi huyo alisema kwamba mnamo tarehe 25 mwezi huu wa Juni 2025, upinzani utawaongoza wakenya kuwakumbuka vijana waliouawa wakati wa Maandamano hayo ya Gen-Zs mwaka uliopita, kwa kuwasha mishumaa nje ya majengo ya bunge.

Kiongozi wa DCP, na aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua alisema serikali ya Kenya Kwanza, inaendelea kupora pesa za wafanyi kazi kutoka hazina ya malipoa ya Uzeeni NSSF, na kuzitumia Kwa miradi ya kibinafsi katika eneo la Bomas.

Picha kwa hisani

Kwa upande wake Kiongozi wa DAP, Eugene Wamalwa alisema kwamba serikali ya Rais Ruto sasa inatumia pesa za ushuru wa nyumba kujenga masoko katika Kaunti mbali mbali kama njia Moja wapo ya mbinu za kuwashawawishi viongozi hasa Magavana,kuunga mkono serikali ya KK, na kuongeza Kwamba ujenzi wa masoko ni jukumu la serikali za ugatuzi.

Viongozi hao waliwahutubia wananchi katika soko la Kwajiwa mjini Malindi, huku msafara huo ukisimama eneo la Matsangoni, Chuo kikuu Cha Pwani mjini Kilifi, na mji wa Mtwapa.

 

Taarifa ya Eric ponda

Continue Reading

Trending