News
Kesi ya Pembe za Ndovu kuendelea katika Mahakama ya Mombasa

Raia wawili wa taifa la Burundi wamefikishwa katika Mahakama ya Mombasa kwa madai ya kumiliki na kujaribu kusafirisha pembe za Ndovu zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 12.
Gakiza Sulemani na Nkunubumwe Celecius walifikishwa mbele ya Hakimu mkaazi Mwandamizi David Odhiambo kwa makosa ya kushughulikia vipande 27 vya pembe za Ndovu kinyume cha sheria.
Pembe hizo zilizokadiriwa kuwa na uzito wa kilo 62.85, zilinaswa katika eneo la Miritini kaunti ya Mombasa kufuatia operesheni ya kijasusi iliyotekelezwa na maafisa wa Huduma ya Wanyamapori nchini KWS.
Washukiwa hao pia walikabiliwa na shtaka la pili la kumiliki sehemu za wanyamapori walioko kwenye hatari ya kutoweka bila idhini ya serikali kinyume na sheria ya mwaka 2013.
Washukiwa hao hata hivyo walikana mashtaka hayo huku Mahakama ikiwaachilia kwa dhamana ya shilingi milioni 4 kila mmoja na mdhamini wa kiasi sawa na hicho pamoja na masharti ya kuwasilisha pasipoti zao na majina ya Wakenya wawili wa kuwawajibikia.
Kesi hiyo itatajwa tena mnamo tarehe 20 mwezi huu Agosti.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.
Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.
Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.
Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.
Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.
Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.
Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.
Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
News18 hours ago
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi
-
Sports17 hours ago
Kocha wa Uingereza Thomas Tuchel akataa madai ya “laana” huku akilenga kuvunja ukame wa miaka 60 wa mataji makubwa
-
Sports17 hours ago
Lionel Messi afunga mabao mawili akiiongoza Argentina, huku Uruguay, Colombia na Paraguay wakifuzu Kombe la Dunia 2026