Sports
Kenya Harlequins Tayari Kwa Msururu wa Chistie 7s Nairobi

Kocha Mkuu wa kilabu ya Kenya Harlequins na mchezaji wa zamani wa Shujaa, Samuel Odongo, ameonya kuwa wako tayari kwa vita wakati wa toleo la 59 la Christie 7s litakaloanza hii leo, Agosti hadi 17 katika uwanja wa RFUEA.
Baada ya msururu wa Prinsloo Sevens,kikosi hicho kimepangwa Kundi A wakiwa pamoja na mabingwa wa Prinsloo mara mbili mfululizo, Strathmore Leos, Zetech Oaks na MSC Rugby.
Harlequins, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi ya saba kwenye msururu wa National Sevens wakiwa na pointi 24, wameweza kumaliza katika nafasi ya sita kwenye Driftwood na Prinsloo Sevens. Odongo, anayelenga kutetea taji la jumla la Quins, alibainisha kuwa ushindani utakuwa mkali, hasa ikizingatiwa kwamba migawo miwili ya mwanzo tayari imetoa mabingwa tofauti na pia kuongezwa kwa kikosi maalum cha Uganda, Ruga Ruga.
“Mashindano haya yatakuwa magumu. Migawo miwili iliyopita imeshuhudia mabingwa wawili tofauti, na pia kuwa na Ruga Ruga kunaleta upekee wa aina yake. Itakuwa wikendi yenye msisimko wa kupanda na kushuka, hasa kwa timu kubwa kushangazwa, na tunatumai hatutajikuta kwenye kapu hilo,” alisema Odongo.
Kauli yake iliungwa mkono na nahodha wa Quins na nyota wa zamani wa U-20, Richel Wangila, ambaye alionyesha kujiamini licha ya mwanzo wa msimu usio wa kuridhisha.
“Tumeendelea kujijenga na kuwa wavumilivu. Hata baada ya matokeo yasiyoridhisha kwenye misururu miwili ya mwanzo, tuko tayari kuwapatie mashabiki burudani ya kuvutia. Tunakazana kushinda mchezo wa kwanza, kisha kuchukua kila mechi inavyokuja, huku lengo kuu likiwa ni kufika fainali na kulinyakua kombe,” alisema Wangila.
Mashindano hayo ya siku tatu yanaanza leo kwa michuano ya vijana asubuhi, ikifuatiwa na mashindano ya wastaafu jioni. Hatua kuu ya Christie Sevens inaanza kesho, ambapo inatarajiwa kushuhudiwa mchezo wa kasi wa raga huku timu zikipambana kwa alama muhimu za msururu.
Sports
Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.
WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.
Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.
Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:
-
Urusi
-
Sri Lanka
-
Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota
-
Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)
Sports
Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.
Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.
“Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.
Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.
Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.
“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”
Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.
“Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.
Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.
Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.
-
Entertainment8 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment20 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News17 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni