Connect with us

News

KEMNAC, yaunga mkono taifa la Tanzania kutoruhusu Wanaharakati wa Kenya

Published

on

Baraza kuu la mashauri ya Waislamu nchini KEMNAC limeunga mkono taifa la Tanzania kwa kutoruhusu Wanaharakati wa kijamii na baadhi ya viongozi kutoka Kenya kuingilia siasa za taifa hilo.

Mwenyekiti wa baraza hilo Sheikh Juma Ngao, alisema Tanzania kuna amani na utulivu mkubwa ikilinganishwa na mataifa mengine ya Afrika mashariki.

Sheikh Ngao, aliwataka vijana wanaotengeneza maudhui na semi za kutisha na kumkejeli Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kukoma mara moja, akisisitiza kuwa ni kumkosea heshima na kumdhalilisha kiongozi huyo bila sababu za msingi.

Sheikh Ngao alisema taifa la Kenya limejaa ukabila na chuki za kisiasa tofauti na na taifa la Tanzania ambalo linajulikana kuwa taifa lenya amani na uzalendo huku akiwataka wakenya kuimarisha umoja na mshikamano kabla ya kuenda kutafutia amani nchi zengine.

“Tanzania tangu ipate uhuru wake, jeshi lake halijathubutu kupindua nchi hapa waliothubutu, hakujaandamanwa kuvamia bunge na kulichoma hapa ilifanyika, hakujapiganwa mpaka kukapatikana Waziri mkuu wa nchini kule kulipatikana Waziri mkuu kisheria, kwa hivyo Kenya huweze kuwafundisha watu wa Tanzania mambo ya Amani”, alisema Sheikh Ngao.

Kwa upande wake, Abubakar Amin Al’alawi, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Baraza hilo, aliwataka viongozi wa kidini, kijamii, na wazazi kuwaelimisha vijana na watoto wao kuhusu maadili mema ili kuepuka chuki miongoni mwa mataifa haya mawili.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Serikali yaombwa kuondoa miili 400 hospitali ya Malindi

Published

on

By

Kamati ya afya ya bunge la seneti sasa imetoa wito kwa serikali kuu kuiondoa miili zaidi ya 400 ambayo inaendelea kuhifadhiwa katika makafani ya hospitali ya Malindi kaunti ya Kilifi baada ya kufukuliwa katika msitu wa Shakahola.

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo, seneta wa kaunti ya Bungoma David Wakoli, alisema maiti hizo zimezuia serikali ya kaunti ya Kilifi kuendeleza ujenzi wa makafani mpya katika hospitali hiyo.

Wakoli alisema ikiwa serikali itazingatia hilo basi serikali ya kaunti ya Kilifi itaweza kujenga makafani hiyo bila changamotoz zozote.

“Tunataka kuiomba serikali kuu kuruhusu serikali ya kaunti ya Kilifi kuendeleza ujenzi huo, na serikali inapaswa kutafuta eneo maalumu la kuhifadhi na kuizika miili hiyo’’ Alisema Wakoli

Hii ni baada ya serikali kutenga fedha katika bajeti ya mwaka jana ili kujenga makafani mpya kushindwa kuendeleza ujenzi huo kutokana na miili ambayo bado haijatambuliwa.

Ni kauli ambayo iliungwa mkono na seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo ambaye aliitaka serikali kuu kukamilisha shughuli ya uambatanishaji wa chembechembe za msimbojeni-DNA, ili kupeana miili hiyo kwa wapendwa wao kabla ya kuanza kufukua miili mingine katika eneo la Kwa Binzaro huko Shakaholo.

“Kule Shakahola tumeona watu wanaendelea kufa na wengine kuzikwa, kwahivyo tunaomba zile maita ambazo ziko hapa ziweze kuondolewa na serikali kuu maana hakuna nafasi,’’ alisisitiza Madzayo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Rais Ruto amteua Amani Yuda Komora kuwa Mwenyekiti wa NPSC

Published

on

By

Rais William Ruto amemteua Amani Yuda Komora kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kitaifa ya Huduma ya Polisi (NPSC) na Angeline Yiamiton Siparo kuwa mwanachama.

Uteuzi huo unafuatia mahojiano ya hivi majuzi yaliyofanywa na Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) kati ya Julai 1 na Julai 3 2025, baada ya kuorodhesha wagombea wanane wa uwenyekiti na 11 wa wajumbe.

Wawaniaji walitakiwa kuwasilisha kitambulisho halisi cha kitaifa, hati za masomo, na idhini halali kutoka kwa mashirika ya serikali.

Stakabadhi nyingine ilikuwa ni pamoja na nyaraka za mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini (KRA), tume ya maadili na kupambana na ufisadi (EACC), fomu maalum kutoka kwa mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa jinai (DCI), bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HELB) na ofisi yoyote iliyosajiliwa ya marejeleo ya mikopo.

Wale walio na shahadi ya digrii za mataifa ya kigeni walilazimika kuwasilisha barua za utambulisho kutoka kwa tume ya elimu ya vyuo vikuu.

Shughuli ya uteuzi ilianza mnamo mwezi Februari baada ya kujiondoa kwa tume ya awali, inayoongozwa na Eliud Kinuthia, ambaye muhula wake wa miaka sita ulimalizika mapema mwaka huu wa 2025.

Iwapo itaidhinishwa na Bunge, NPSC itajumuisha Komora kama Mwenyekiti na wanachama watano wakiwemo, Peris Muthoni Kimani, Edwin Cheluget, Benjamin Juma Imai, Collete Suda na Angeline Yiamiton Siparo

Komora ni naibu mwenyekiti wa zamani wa tume ya kutathmini mishahara na marupurupu ya wafanyakazi wa umma (SRC), na hapo awali alikuwa na majukumu ya juu ya rasilimali watu katika Mamlaka ya Bandari KPA na KRA.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending