Entertainment
Kelechi: Kama Content Haibebi Bila Mimi, Rethink the Plan – Clout Si Career

Kelechi Afrikana, kwa mara nyingine tena ametoa ujumbe mzito kwa wale wanaotafuta umaarufu (clout) kupitia jina lake, akisisitiza kuwa muziki unapaswa kuwa msingi wa mafanikio ya kweli – si kelele za mitandaoni.
Kupitia chapisho kwenye Facebook, Kelechi alitoa kauli kali iliyogusa si tu maisha ya wasanii, bali pia maudhui ya mitandaoni yanayozidi kutawaliwa na mbinu za kuvutia macho badala ya vipaji halisi.
Wasanii wengi wamekuwa wakikumbana na wimbi la “drag culture” – watu wanaotengeneza maudhui kwa kumhusisha na kumchafua bila sababu, ili kuvutia wafuasi au kuteka macho ya mtandao lakini Kelechi ameweka wazi kwamba kuvuma si sawa na kustahimili, na mafanikio ya kweli yanatokana na kazi halisi, si drama ya kupangwa.
“Si lazima utaje jina yangu ndo upate followers bruv 😤 Clout si career — especially when you’re forcing it off someone else’s wave. Kama content haibebi bila kudrag jina ya mtu, maybe it’s time to rethink the whole plan,” Kelechi alisema.
Kelechi aliwakumbusha wafuasi wake kuwa muziki ni sanaa — na kama kazi yako haiwezi kujisimamia bila kuchomeka jina la mtu mwingine, basi kuna haja ya kutathmini upya dhamira yako.
Post ya Kelechi ilikuwa pia ya shukrani na matumaini. Kelechi aliwashukuru mashabiki wake na hasa @mummiefrancie, kwa kuonyesha upendo mkubwa kwa wimbo wake mpya “Litapita”.
Aliandika: “Mkinisisupport walai naeza fika mbali 🙏🔥 Shukran sana @mummiefrancie Francie kwa kuvybea na kuonyesha upendo kwa ngoma yangu “Litapita” 🥹❤️Support kama hii inanipa nguvu ya kuendelea, na najua naweza go far with y’all behind me!”
Chapisho la Kelechi ni zaidi ya rant ya mtandao – ni tamko la msanii anayeamini katika kazi yake, anayetaka kuona muziki wake ukithaminiwa kwa ubora wake, si kwa kiki.
Ikumbukwe kuwa baadhi ya wasanii wamekuwa wakitumia kiki kusukuma kazi zao. Hata hivyo, Kelechi anatufundisha thamani ya vitu vya kweli: kazi, maadili, na kuaminiana.
Kelechi alisema: “Let the music speak — not the noise.” 🎧🚫
Entertainment
Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.
Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.
Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.
Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.
Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.
Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.
Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.
Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.
Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.
Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.
Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.
Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.
Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.
Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.
Chanzo: BBC
Entertainment
Justin Bierber Arejea na Album Mpya ‘SWAGG’

Msanii nyota wa muziki wa kimataifa, Justin Bieber, hatimaye ameachia rasmi albamu yake mpya na ya saba kwa jina “Swag”, ikiwa ni albamu yake ya kwanza tangu mwaka 2021 alipotoa Justice. Albamu hii imetoka leo na tayari imeanza kutikisa majukwaa mbalimbali ya muziki duniani.
Swag imejumuisha mastaa kadhaa akiwemo Gunna, Sexyy Red, Cash Cobain, pamoja na wasanii wengine wa kizazi kipya.
Albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 20 na tayari baadhi ya vibao kama “Go Baby”, “Soulful” na Butterflies “zimeanza kupokelewa vizuri kwenye mitandao ya Spotify, Apple Music na YouTube.
Hii ni mara ya kwanza kwa Bieber kuachia albamu tangu alipopata matatizo ya kiafya mwaka 2022 yaliyosababisha asitishe ziara yake ya kimataifa ya Justice World Tour ambayo ilikuwa iendelee hadi mwaka 2023.
Ziara hiyo ilisitishwa mnamo Septemba 2022 baada ya Bieber kupatwa na maradhi ya Ramsay Hunt Syndrome, ugonjwa uliomsababishia kupooza upande mmoja wa uso.
Kwa kipindi cha miaka minne bila kazi mpya, mashabiki wa Justin Bieber duniani wamekuwa wakimsubiria kwa hamu ujio wa kazi mpya kutoka kwake. Kupitia Swag, msanii huyo ameonyesha kurejea kwa nguvu na ubunifu wa hali ya juu, huku akiwa katika hali nzuri kiafya na kisaikolojia.
Taarifa na Francos Mzungu