News
Karua, Aomba Mahakama Kumuachilia Bessigye kwa Dhamana

Kiongozi wa Chama cha People’s Liberation Party, PLP nchini Kenya Martha Karua, aliwasili nchini Uganda katika juhudi za kumuakilisha Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Bessigye anayetuhumiwa kwa kosa la Uhaini.
Bessigye alikamatwa nchini Kenya miezi sita iliyopita na kuwasilishwa Mahakamani licha ya hali yake ya kiafya kuonekana kudhoofika.
Akiwasilisha hoja yake Mahakamani, Karua ameitaka Mahakama hiyo kumuwachilia Bessigye kwa dhamana ikizingatiwa kwamba amekuwa akizuiliwa kwa zaidi ya siku 180 korokoroni bila ya kupata haki.
Kinyume na matukio ya hivi majuzi nchini Tanzania ambako alizuiliwa kwa muda wa saa sita na kisha kurejeshwa nchini Kenya, Kiongozi huyo chama cha PLP, alilakiwa Mahakamani kwa shangwe na nyimbo za ukombozi, kabla ya kupewa nafasi na Mahakama kuwasilisha hoja yake.
Safari yake ya kwenda nchini Uganda kuhudhuria kesi hiyo, inatokea wiki mbili tu baada ya kutibuka kwa jaribio lake la kutaka kumuakilisha kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, ambapo yeye na Wanaharakati wengine wa haki za binadamu walizuiliwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kabla ya kurejeshwa nchini Kenya.
Tukio hilo limezua mashambulio makali ya mitandaoni miongoni mwa kizazi cha sasa cha Gen Z kuishtumu Tanzania kwa madai ya kudhuliwa kwa Mwanaharakati Bonifance Mwangi na mwenzake Agathar Atuhaire kutoka nchini Uganda.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Mudavadi: Mazungumzo yanaendelea kuhusu mzozo wa Kenya na Tanzania

Mzozo kati ya Kenya na Tanzania umeanza kutokota kufuatia ilani iliyotolewa siku ya Jumanne Julia 29, na serikili ya Muungano wa Jumhuri ya Tanzania.
Serikali hiyo ya Tanzania kupitia Waziri wa Biashara na viwanda nchini humo Selemani Jefo ilitoa ilani ya kuwazuia wafanyibiashara wa kigeni kuendelea kufanya baadhi ya biashara katika taifa hilo.
Kutokana na hilo, Waziri wa masuala ya kigeni nchini Musalia Mudavadi alisema juhudi zimeanza za kuishawishi serikali ya Tanzania kuondoa vikwanzo hivyo na kwamba Rais William Ruto anafanya mazungumzo na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu suala hilo.
“Rais William Ruto ambaye ni Mwenyekiti wa Jumaiya ya Afrika Mashariki anafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na mwafaka utapatikana kwani pia suala la diplomasia ni mwafaka na hii tatizo tutatua kama serikali kupitia mazungumzo ya kidiplomasia”, alisema Mudavadi.
Kwa upande wake Waziri wa biashara na viwanda nchini Lei Kinyanjua alionya kwamba huenda serikali ya Kenya ikachukua hatua sawa na hiyo dhidi ya Tanzania iwapo taifa hilo la Afrika Mashariki halitaangazia upya vikwanzo hivyo.
Mzozo huo wa kidiplomasia umejiri siku moja tu baada ya Waziri wa biashara na viwanda nchini Tanzania Selemani Jafo kutangaza kwamba serikali ya Tanzania imepiga marufuku wafanyibiashara wa kigeni dhidi ya kufanya biashara ndogo ndogo nchini humu ili kuruhusu watanzania kujiimarisha kiuchumi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Ethekon: Sheria haijafafanua taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeweka wazi kwamba hakuna sheria inayofafanua misingi na taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi.
IEBC, ilieleza kwamba suala hilo ni kinyume cha Katiba na ubaguzi ikilinganisha hatua hiyo na uamuzi uliyotolewa na Mahakama kuu kuhusu kesi iliyowasilishwa Mahakamani na Taasisi ya Katiba dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria mkuu kwa kuambatana na sheria ya uchaguzi ya 2011.
Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon, IEBC ilisema kutokana na kwamba hakuna mfumo wa sheria wa kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi, wakenya wanaweza kutumia kipengele cha 104 cha Katiba na kuwarudisha nyumbani Wawakilishi wadi.
Aidha alisema wakati bunge la kitaifa likifanya marekebisho ya sheria kuruhusu kurudishwa nyumbani Wawakilishi wadi, hakuna mwafaka wowote uliafikiwa wa kuruhusu wabunge kurudishwa nyumbani iwapo wamekosa kuwajibika.
Hata hivyo Tume hiyo imeahidi kuwajibika kikamilifu katika suala hilo huku ikisema tayari imeliandikia barua bunge la kitaifa kuibuka na sheria ya kuwarudisha nyumbani wabunge wasiowajibika.
Haya yamejiri kufuatia malalamishi yaliowasilishwa na baadhi ya wakenya wanaotaka baadhi ya wabunge na maseneta kurudishwa nyumbani wa hivi karibuni akiwa Mwakilishi wa Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris akituhumiwa kuvunja sheria na kukiukaji wa Katiba lakini uamuzi wa Tume ya IEBC ni afuani kwake.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi