Business
KAHC: Kenya Yaweza Kukosa Watalii Milioni 5 Kufikia 2027

Muungano wa wahudumu wa hoteli na wapishi nchini (KAHC) umesema huenda Kenya ikakosa kufikia lengo la watalii millioni 5 ifikapo mwaka 2027 iwapo maandamano yanayoshughudiwa mara kwa mara humu nchini hayatasitishwa.
Kwa mujibu wa viongozi wa muungano huo, maandamano hayo yamewafanya wageni wengi kutoka mataifa ya kigeni kusitisha safari zao za kuzuru Kenya, hali inayoathiri sekta ya utalii na uchumi kwa ujumla.
Mwenyekiti wa Muungano wa Wamiliki wa Hoteli na Mikahawa nchini (KAHC) Chris Musau, anasema kuwa taswira ya nchi kimataifa imeathirika, na hali hiyo inaweza kupunguza mapato ya sekta ya utalii ambayo ni miongoni mwa vyanzo vikuu vya fedha za kigeni kwa taifa.
Musau aidha anaitaka serikali kuanzisha mazungumzo na vijana wa kizazi cha Gen Z kutafuta suluhu ya migogoro iliyopo ili kurejesha hali ya utulivu nchini.
Business
Kanisa Katoliki lahimiza umuhimu wa Kilimo

Kasisi wa Kanisa Katoliki jimbo la Malindi Misheni ya Mere kaunti ya Kilifi, Blaise Kamau Andrew ametoa wito kwa wenyeji wa Pwani kuwekeza zaidi katika kilimo cha kisasa ili kupata chakula cha kutosha na kilicho bora.
Akizungumza katika eneo la Kwa Ndomo eneo bunge la Malindi, Kasisi Kamau aliesema ikiwa Wapwani watatia juhudi katika sekta ya kilimo huenda kukawa na mavuno mengi na chakula cha kutosha ili kudhibiti njaa wakati wa kiangazi.
Kasisi Kamau pia aliwashinikiza kuchimba visima vingi vya maji ili panapokosekana mvua kuwe na maji ya kutosha ya kuendeleza kilimo nyunyizi.
“Chibeni visima ili usiwe mkulima wa kungojea tu mvua ya mwenyeji Mungu.Tufanyeni bidi wengi wenu wana Ng’ombe, wengi wenu wana mbuzi uza Ng’ombe mbili, chimba kisima maji hayako mbali sana ili mvua ikikatika bado mnaendeleza kilimo nyunyizi’’, alisema Kasisi Kamau.
Ni kauli ambayo imeungwa mkono na msimamizi wa kitengo cha chakula na Kilimo katika benki ya Equity tawi la Nairobi, George Macharia ambaye alisema ili kuimarisha uchumi wa Kenya ni lazima Wapwani na wakenya kwa jumla wakumbatie kilimo cha kisasa kupitia mfumo wa teknolojia.
“Ili tuweze kupanua uchumi ni lazima tuwekeze katika kilimo na tuhakikishe tunatumia kilimo cha kisasa cha kiteknolojia’’, Macharia aliwasihi Wakulima.
Taarifa ya Janet Mumbi
Business
Kanda ya Pwani kuimarika kupitia Kilimo cha kisasa

Kanda ya Pwani inatarajiwa kuimarika zaidi kupitia Kilimo cha kisasa kinachotekelezwa kupitia mfumo wa teknolojia.
Hii ni kupitia mikakati inayoendelezwa na Agitech Seedlings kuhakikisha Wakulima na Wenyeji wa Kanda ya Pwani wanakumbatia Kilimo cha kisasa kama maeneo mengine nchini.
Akizungumza na Coco FM katika maonyesho ya Kilimo cha kisasa na uzinduzi wa tawi jipya la Agitech Seedling katika eneo la Kwa Ndomo mjini Malindi kaunti ya Kilifi, Mkurugenzi wa Agitech Seedlings Peter Karanja Ndung’u alieleza sababu za kuanzisha Kilimo hicho cha kisasa katika ukanda wa Pwani.
Karanja pia alisema wanapania kuhakikisha wenyeji wa Pwani wanahamasishwa ipasavyo na hata kuonyeshwa namna ya kufanya Kilimo hicho hapa pwani.
“Kupitia hamasa ambazo tunatoa kwa wakulima na wenyeji wa Pwani kwa jumla tunatarajia kuwa Kilimo kitaanza kuimarika na kuondoa dhana ambayo imekuwepo kwamba eneo la Pwani linatambulika pekee kwa masuala ya uvuvi’’, alisema Karanja.
Vilevile, Karanja alisema kuna haja ya Wakulima kutunza ardhi zao kwa kuhakikisha zina rutuba ya kutosha ili kuzalisha chakula kwa wingi na bora.
Taarifa ya Janet Mumbi